SALVA KIIR MAYARDIT AWASILI NCHINI NA KULAKIWA NA DKT. CHANA
Waziri wa
Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana na Rais wa Sudan Kusini Mhe.
Salva Kiir Mayardit wakikagua gwaride la heshima, tarehe 23 Novemba, 2023 mara
baada ya kuwasili nchini.
Waziri wa
Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana na Mgeni wake Rais wa Sudan
Kusini Mhe. Salva Kiir Mayardit mara baada ya kuwasili nchini, tarehe 23
Novemba, 2023 Jijini Arusha.
Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir Mayardit amewasili nchini
tarehe 23/11/2023 na kupokewa na Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt.
Pindi Chana kushiriki Mkutano wa Kawaida wa 44 wa Jumuiya ya Afrika Mashariki
unaofanyika Jijini Arusha.
Mara ya mwisho Rais Salva Kiir kuja nchini ilikuwa April 15,
2016 ambapo alikutana na aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Hayati Dkt. John
Pombe Magufuli kwa ajili ya utiaji saini wa Mkataba wa Sudani Kusini kujiunga na
Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Mkutano huo unahudhuriwa na Wajumbe kutoka nchi zote
wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambazo ni mwenyeji Tanzania, Burundi,
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Kenya, Uganda, Rwanda, na Sudan Kusini.
Comments
Post a Comment