WAZIRI CHANA AIPONGEZA NMB KWA KUTOA HUDUMA ZINAZOIGUSA JAMII
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Balozi Dkt Pindi Chana akiwa katika picha ya pamoja na Wanasheria Binafsi katika mkutano uliofanyika leo tarehe 10 Novemba Jijini Dar es Salaam .
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Balozi Dkt Pindi Chanaajiongea na Wanasheria Binafsi kwenye mkutano uliofanyika leo tarehe 10 Novemba Jijini Dar es Salaam .
Na Lusajo Mwakabuku –
WKS
Waziri wa Katiba n Sheria
Mhe.Balozi Dkt Pindi Chana Ameshiriki Mkutano wa NMB na Taasisi za Sheria za
Mkoa wa Dar es Salaam na Kuipongeza Benki hiyo kwa kuendelea kufanya kazi kwa
Weledi na kuiomba kuendelea kushiriki kwenye Huduma mbali mbali zinazogusa jamii.
Akisoma hotuba yake, Waziri Chana
ambaye alikuwa Mgeni Rasmi katika hafla hiyo aliwaomba NMB na Wanasheria kuunga
mkono Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (Samia Legal Aid Campaign)
kwa hali na mali kwa ikiwa ni sehemu ya utekelezaji kurudisha kwa jamii (Corporate
Social Responsibility).
Waziri Chana aliongeza kuwa
kampeni hii inakusudia kutoa elimu ya sheria nchi nzima pamoja na msaada wa
kisheria itakayojenga taifa la watu wenye ufahamu wa sheria hivyo watu wataacha
kukopa mikopo ya kausha damu au vikoba vya kuficha fedha uvunguni na kuja
kukopa benki ambapo napo watahitaji huduma ya wakili kuthibisha mikopo yao.
Mkutano huo ulioudhuriwa na
Waziri wa Viwanda na Biashara Mh Omary Said Shaabani ambae amesema NMB imekua
chachu kwa maendeleo ya ya Viwanda na Biashara kwa ujumla na kuitaka iongeze
huduma kwa upande wa Zanzibar.
Aidha Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB Ruth Zaipuna
ameishukuru Serikali kwa kuendelea kuweka mazingira rafiki yanayowezesha huduma
za Benki kukua kwa kiasi kikubwa.
Comments
Post a Comment