WAZIRI CHANA ASHIRIKI KIKAO CHA BARAZA LA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akishiriki Mkutano wa Kawaida wa 44 wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki, tarehe 22 Novemba, 2023 Jijini Arusha.
Waziri
wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akishiriki Mkutano wa Kawaida
wa 44 wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki, tarehe 22 Novemba,
2023 Jijini Arusha.
Waziri
wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana anashiriki Mkutano wa Kawaida
wa 44 wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyikia Jijini
Arusha.
Mkutano
huo ulioanzia katika Ngazi ya Wataalam waliokutana Jijini Arusha kuanzia tarehe
18 - 20 Novemba, 2023 na ukafuatiwa na Kikao cha Makatibu Wakuu kilichofanyika
tarehe 21 Novemba 2023, kinakamilishwa na Mkutano wa 44 wa Baraza la Mawaziri
ulioanza leo tarehe 22 Novemba 2023.
Masuala
yanayojadiliwa katika Mkutano huo wa wataalam ni pamoja na Taarifa ya
Utekelezaji wa maamuzi na maelekezo ya mkutano cha Baraza la Mawaziri kwa
kipindi cha kuanzia tarehe 1 Julai, 2022 hadi 24 Novemba, 2023; Taarifa ya
utekelezaji wa maazimio na maelekezo ya Wakuu wa Nchi wa Jumuiya kuhusu;
Majadiliano ya Jamhuri ya Somalia kujiunga na Jumuiya; Hatua iliyofikiwa katika
kutafuta amani Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika maeneo ya
mchakato wa kijeshi na uongezaji muda wa mkataba wa SOFA; Hali ya Kifedha ya
Mfuko wa Akiba wa Jumuiya ya Afrika; majadiliano ya Katiba kuhusu Katiba ya
Fungamano la Kisiasa Afrika Mashariki; Tathmini ya miswada iliyopitishwa na
Bunge la Afrika Mashariki na; Utoaji wa Tuzo kwa washindi wa mashindano ya
Uandishi wa insha kwa wanafunzi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Mkutano
huo unahudhuriwa na Wajumbe kutoka nchi zote wanachama wa Jumuiya ya Afrika
Mashariki ambazo ni mwenyeji Tanzania, Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya
Congo (DRC) Kenya, Uganda, Rwanda, na Sudan Kusini.
Comments
Post a Comment