Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akitoa ufafanuzi kwenye kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria tarehe 07 Novemba, 2023 Jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu akitoa ufafanuzi mbele ya Kamati ya Kudumu ya Utawala, Katiba na Sheria tarehe 07 Novemba, 2023 Jijini Dodoma.
Wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na
Sheria wakisikiliza taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Tume ya Haki za
Binadamu na Utawala bora tarehe 07 Novemba, 2023 Jijini Dodoma.
Na George Mwakyembe - WKS Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi
Dkt Pindi Chana amewasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Tume za Haki
za Binadamu na Utawala bora kwenye Kamati ya Kudumu ya bunge ya Utawala, Katiba
na Sheria. Katika taarifa hiyo Mhe. Chana amefafanua kuwa utekelezaji wa
majukumu ya Tume ni ya mtambuka kwani yanagusa maisha ya
binadamu ya kila siku.
Mhe. Chana
amewasilisha taarifa hiyo tarehe 07 Novemba, 2023 katika ukumbi wa Bunge Jijini
Dodoma. Akifafanunua kwenye kikao Mhe. Chana amebainisha kuwa Tume ya Haki za
Binadamu na Utawala Bora ni taasisi ambayo ni ya Muungano na imekuwa
ikishughulikia masaula yote ya haki za binadamu Tanzania Bara na Tanzania
Zanzibar.
Naye Mwenyekiti
wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu
amewambia wajumbe wa Kamati hiyo kuwa Tume imekuwa ikisimamia masuala ya haki
za binadamu pamoja na utawala bora lakini changamoto wanayopata ni upungufu wa
watumishi. Pia Tume imekuwa ikipata changamoto ya kutokupata taarifa pindi
matukio ya ukiukwaji wa haki za binadamu yanapotokea.
Akichangia
kwenye uwasilishwaji Makamu Mwenyekiti wa Tume Mohamed Hamad amewashukuru
wajumbe kwa kuwapa ushirikiano lakini pia kuwaongezea bajeti ukilinganisha na
miaka ya nyuma na tayari wamefungua ofisi nyingine Zanzibar ili kuhakikisha
tunashughulikia msauala ya haki kwa pamoja.
Comments
Post a Comment