DKT. CHANA ATAKA WATUMISHI KUFANYA KAZI KWA KUZINGATIA MASLAHI YA TAIFA

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana kwenye picha ya pamoja na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya RITA, 22 Desemba, 2023 Jijini Arusha.

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akihutubia wakati akifungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya RITA, 22 Desemba, 2023 Jijini Arusha.

XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

Na William Mabusi – WKS Dodoma

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana ametoa wito kwa watumishi wa umma kufanya kazi kwa weledi na uadilifu kwa kuzingata maslahi mapana ya Serikali na Taifa kwa ujumla.

Dkt. Chana ameyasema hayo wakati akifungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa ofisi ya RITA tarehe 22 Desemba, 2023 linalofanyika Jijini Arusha. Baraza hilo linafanyika ikiwa ni utekelezaji wa Sheria ya ajira na Mahusiano kazini.

Amesema, “huduma ya usajili wa matukio muhimu ya binadamu na Takwimu mnazotoa ni huduma zinazowagusa wananchi moja kwa moja. Hivyo, mkiwa wafanyakazi mlioaminiwa na Serikali ya Tanzania endeleeni kutekeleza majukumu yenu kwa weledi na uadilifu kwa kuzingata maslahi mapana ya Serikali na Taifa kwa ujumla.”

Amezitaja huduma zinazotolewa na RITA kuwa ni pamoja na usajili wa Vizazi, Vifo, Ndoa, Talaka na Watoto wa kuasili, Usimamizi wa mirathi, Usajili wa Bodi za Wadhamini, Kuandika na kuhifadhi wosia miongoni mwa zingine.

Dkt. Chana amemshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa utekelezaji wa falsafa ya R 4 hususan kwenye maboresho ya huduma zinazotolewa na Wakala wa RITA huku akiuagiza uongozi wa RITA kushughulikia changamoto mbalimbali za watumishi. “shughulikieni changamoto za wafanyakazi waweze kufanya kazi kwa furaha na ufanisi kwa kuwa mtumishi akiwa na furaha katika kazi ni wazi utendaji wake utakuwa wenye tija.”

Aidha, Dkt. Chana amehimiza umoja miongoni mwa wafanyakazi wa ofisi ya RITA akiwataka wajenge Utumishi wa Umma wenye kuzingatia Kanuni za Maadili ya Utumishi, kupinga rushwa na kuheshimu sheria.


Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA