KUPIGA VITA RUSHWA NI JUKUMU LETU SOTE – MHE. PINDI CHANA.
Waziri
wa Katiba na Sheria Mhe. Pindi Chana akiongea na Wananchi kwenye Uzinduzi wa Maadhimisho ya ya siku ya Maadili na Haki za Binadamu Kitaifa yalifanyika uwanja wa Jamhuri leo
tarehe 03 Desemba 2023 Jijini Dodoma
Waziri
wa katiba na sheria Mhe. Pindi Chana akiwa na viongozi meza kuu
kwenye Uzinduzi wa Maadhimisho ya
ya siku ya Maadili na Haki za
Binadamu Kitaifa yalifanyika uwanja wa
Jamhuri leo tarehe 03 Desemba 2023 Jijini Dodoma
Waziri
wa Katiba na Sheria Mhe. Pindi Chana akiwa katika picha ya pamoja na mshindi wa
mbio za Sepesha Rushwa Marathoni kilomita
21 kwa upande wa wanawake leo tarehe 03
Desemba 2023 Jijini Dodoma.
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Na George Mwakyembe – WKS Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana
amesema kuwa uwepo wa vitendo vya rushwa kunaifanya Serikali kushindwa
kutekeleza majukumu yake ipasavyo, kushindwa kuwahudumia wananchi, miradi ya
maendeleo kushindwa kufanyika au
kufanyika kwa kiwango cha chini kutokana
na fedha zinazotengwa kutekeleza
miradi hiyo kuingia katika mikono ya watu wachache.
Mhe. Chana ameyasema hayo alipokuwa akizindua Maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu Kitaifa yaliyofanyika tarehe 03 Desemba, 2023 kwenye Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.
“Maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu ni fursa nzuri ya kujitafakari tulikotoka na tunakokwenda katika jitihada za kuimarisha uchumi pamoja na uboreshaji wa huduma kwa wananchi.” Alisema.
Akitoa salaam, Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Jaji Mstaafu Mhe. Mathew Mwaimu amesema Tanzania imepiga hatua kubwa sana katika kusimamia masuala ya haki za binadamu na hii inadhihirishwa na Mhe. Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa mstari wa mbele katika kupinga vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu ikiwemo unyanyasaji, rushwa na ukatili wa kijinsia.
Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na wananchi kutoka mikoa mbalimbali nchini yakiambatana na mbio ndefu na fupi zilizoitwa Sepesha Rushwa Marathoni zikiwa na lengo la kupinga vitendo vya rushwa nchini. Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni “Zingatia Maadili, Utu, Uhuru na Haki kwa watu wote kwa Maendeleo ya Endelevu.”
Maadhimisho hayo yanaadhimishwa sambamba na maadhimisho ya miaka 75 ya Tamko la Haki za Binadamu (Universal Declaration of Human Rights) ambayo huadhimishwa kila tarehe 10 Desemba ya kila mwaka hivyo siku hiyo ndiyo itakuwa kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu Kitaifa.
Comments
Post a Comment