TANZANIA IMESAJILI NA KUTOA VYETI VYA KUZALIWA KWA WATOTO ZAIDI YA MILIONI NANE
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt.
Pindi Chana akihutubia wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mpango wa Usajili wa
Watoto wa Umri chini ya miaka mitano, Desemba 08, 2023 katika viwanja vya
Mbagala Zakhiem Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizira ya Katiba na Sheria Bi. Mary
Makondo akihutubia wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mpango wa Usajili wa Watoto
wa Umri chini ya miaka mitano, Desemba 08, 2023 katika viwanja vya Mbagala
Zakhiem Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt.
Pindi Chana akizindua Mpango wa Usajili wa Watoto wa Umri chini ya miaka
mitano, Desemba 08, 2023 katika viwanja vya Mbagala Zakhiem Jijini Dar es
Salaam.
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Na Lusajo Mwakabuku -
DSM
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amesema kuwa Watoto zaidi ya milioni 8.8 wamesajiliwa na kupatiwa vyeti vya kuzaliwa katika mikoa 26 ya Tanzania Bara kupitia Mpango wa Usajili wa Watoto wa Umri chini ya miaka mitano.
Mhe. Waziri Balozi Dkt. Pindi Chana ameyasema
hayo wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mpango leo Desemba 08, 2023 katika viwanja
vya Mbagala Zakhiem Jijini Dar es Salaam.
Uzinduzi huu unahitimisha Mikoa 26 ya Tanzania bara ambapo Mkoa wa Dar es Salaam unatarajiwa kusajili jumla ya watoto 248,298 na kupatiwa vyeti vya kuzaliwa bila ya malipo kupitia vituo 505 vya usajili ambavyo ni Vituo vya Afya na Ofisi za Watendaji wa Kata.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo amesema, mpango huo ulioanza jijini Mbeya mwaka 2013 na kuhitimishwa jijini Dar es Salaam ikiwa ni jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita ambayo imekuwa ikitenga bajeti ya utekelezaji wa majukumu hayo na kuhakikisha wananchi wanasogezewa huduma katika maeneo wanakoishi.
Ameongeza kuwa, mpango huo ni mfano wa
maboresho kwa kuwa huduma zimesogezwa karibu na wananchi na kutumia teknolojia
ya simu za mkononi ambayo inarahisisha upatikanaji wa takwimu za watoto wengi
wanaosajiliwa ndani ya muda mfupi.
Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri RITA Dkt. Amina Msengwa amesema kuwa mpango huo ulianzishwa na Serikali kupitia RITA kwa kundi hilo la kimkakati la watoto kwani mipango mingi ya maendeleo hutegemea takwimu sahihi na hivyo kupitia mpango huo utawezesha Serikali kupata takwimu sahihi kwa wakati.
Naye Kabidhi Wasii Mkuu Bw. Frank Kanyusi amesema, Lengo la Mpango huo ni kuongeza kasi ya ya Usajili na kutoa vyeti kwa watoto wa Umri chini ya miaka mitano pamoja na kusogeza huduma kwa wananchi kuanzia ngazi ya Kata.
"Chimbuko la mpango huu ni kasi ndogo ya usajili, Serikali kwa kushirikiana na wadau wakaleta mpango huu ili kuongeza kasi ya usajili na utoaji wa vyeti vya kuzaliwa kwa watanzania wote." Amesema.
Pia, amewashukuru wadau mbalimbali wa Kitaifa
na Kimataifa ambao ni Serikali ya Canada, Shirika la kuhudumia watoto duniani
UNICEF, Kampuni ya simu za mkononi Tigo na kuahidi kuendelea na ushirikiano
katika utoaji wa huduma hiyo kwa wananchi.
Comments
Post a Comment