TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA UPATIKANAJI HAKI NCHINI INDIA
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pindi Chana akiwa na wajumbe kutoka Tanzania kwenye Mkutano wa Upatikanaji Haki uliofanyika tarehe 27- 28 New Delhi, India .
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Na,
George Mwakyembe - WKS
Tanzania ni moja kati ya nchi washiriki katika mkutano wa kwanza wa kikanda kuhusu upatikanaji wa msaada wa kisheria, pamoja na Uimarishaji wa upatikanaji Haki katika nchi za ukanda wa kusini.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana ameongoza washiriki kutoka Tanzania katika mkutano huo uliofanyika New Delhi nchini India kuanzia tarehe 27– 28 Novemba 2023 ukiwa unalenga kujadili masuala ya upatikanaji wa huduma za msaada wa kisheria katika kuimarisha upatikanaji haki nchini.
Katika
Mkutano huo washiriki walipata nafasi ya kubadilishana uzoefu juu ya
utekelezaji wa masuala ya huduma za msaada wa kisheria na jitihada mbalimbali
zinazotumika katika kuhakikisha upatikanaji haki katika nchi zao pamoja na
kuimarisha uhusiano na baina nchi washiriki na wadau mbalimbali wa haki
katika ukanda wa kusini.
Comments
Post a Comment