UJENZI WA JENGO LA WIZARA WAFIKIA ASILIMIA 80
0 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Dkt.
Khatibu Kazungu akitembelea na kukagua ujenzi wa jengo la Wizara, tarehe 29
Desemba, 2023 Mji wa Serikali Mtumba.
Mkandarasi Nasiri Nassoro akifafanua jambo wakati akitoa maelezo ya maendeleo ya ujenzi kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Khatibu Kazungu alipotembelea na kukagua ujenzi huo, tarehe 29 Desemba, 2023 Mji wa Serikali Mtumba
01 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Dkt.
Khatibu Kazungu akishauri jambo alipotembelea na kukagua ujenzi wa jengo la
Wizara, tarehe 29 Desemba, 2023 Mji wa Serikali Mtumba.
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Na William Mabusi - WKS Dodoma
Ujenzi
wa jengo la Wizara ya Katiba na Sheria linalojengwa Mji wa Serikali Mtumba
limefikia asilimia themanini (80).
Taarifa
hiyo imetolewa na Bw. Ibrahimu Chatila Mtaalam Mwelekezi kutoka Wakala wa
Majengo Tanzania (TBA) kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Dkt.
Khatibu Kazungu tarehe 29 Desemba, 2023 alipotembelea maendeleo ya ujenzi huo.
Aidha, Bw. Chatila amemtaka Mkandarasi wa ujenzi huo SUMA JKT kutobweteka kwa
hiyo asilimia themanini kwani mradi huo ni miongoni mwa miradi ambayo
Mkandarasi analipwa kwa wakati.
Akitoa
maelekezo baada kukagua maendeleo ya ujenzi huo Dkt. Kazungu amesema “jitihada
mlizoonesha hadi kufikia hatua hii ongezeni bidii na hasa baada ya kupokea
vifaa vyenu vya ujenzi ambavyo bado viko bandarini.”
Kabla
ya kufanya ukaguzi wa ujenzi Dkt. Kazungu akiwa na Menejimenti ya Wizara hiyo
walikutana na kufanya mazungumzo na Wakandarasi kutoka SUMA JKT na Wataalam wa
Majengo kutoka TBA.
Comments
Post a Comment