Wananchi watakiwa kuunga mkono jitihada za Serikali kupinga ukiukwaji wa haki za binadamu
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa katika banda la Wizara ya
Katiba na Sheria kwenye Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za
Binadamu yaliyofanyika leo tarehe 10 Desemba 2023 Jijini Dodoma.
Mgeni rasmi Mhe. Kassim Majaliwa akiwa na viongozi wengine meza kuu kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya Maadili na Haki za Binadamu yalifanyika leo tarehe 10 Desemba 2023 jijini Dodoma.
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akitoa
hotuba kwenye Kilele cha Maadhimisho ya siku ya Maadili na Haki za Binadamu yaliyofanyika
leo tarehe 10 Desemba 2023 Jijini Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Balozi
Pindi Chana akitoa neon la utambulisho kwenye Kilele cha Maadhimisho ya siku ya
Maadili na Haki za Binadamu yaliyofanyika leo tarehe 10 Desemba 2023 Jijini
Dodoma
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Na George Mwakyembe & William Mabusi – WKS Dodoma
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb) ametoa wito kwa
wananchi kuunga mkono jitihada za Serikali ili kuleta matokeo chanya katika
kupinga vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu, rushwa na mmomonyoko wa
maadili akiwataka wanachi wanapobaini vitendo hivyo kutoa tarifa kwenye vyombo
vya sheria ili wahusika wachukuliwe hatua.
Waziri Mkuu ameyasema hayo
alipokuwa akihutubia wakati wa kufunga maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki
za Binadamu Kitaifa leo tarehe 10 Desemba, 2023 hafla iliyofanyika Viwanja vya
Nyerere Square Jijini Dodoma yakiongozwa na kauli mbiu isemayo "Zingatia
maadili, utu, uhuru na haki kwa watu wote kwa maendeleo endelevu."
Mhe. Majaliwa amesema “Wananchi
ninyi ni wadau wakubwa wa kutokomeza rushwa, kukomesha vitendo vya ukiukwaji wa
haki za binadamu. Ili nchi yetu isiwe na vitendo vya rushwa, isiwe na vitendi
vya ukiukwaji wa haki za binadamu nyie mnapaswa kufichua matendo hayo na
kupeleka taarifa kwenye vyombo husika katika kusimamia na kudhibiti matendo
hayo, mwananchi usikubali kutoa rushwa popote unapotakiwa kupata huduma.”
Katika kukabiliana na dhuruma ya rushwa amesema nchi imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwa na Mkakati wa Kitaifa wa kupambana na rushwa ambao hadi sasa umetekelezwa kwa Awamu Tatu na katika hafla hiyo alizindua Mkakati wa Nne wa kupambana na rushwa ili uanze kutumika rasmi huku akiagiza elimu ya utekelezaji wa Mkakati huo iendelee kutolewa ili kuwawezesha wadau wote kuwa na uelewa wa pamoja katika kushiriki kutekeleza Mkakati huo.
Awali akitoa salaam kwenye hafla
hiyo Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) amezishukuru
Wizara na Taaasisi ambazo kwa wiki nzima zimeshiriki kutoa elimu juu ya haki za
binadamu, rushwa, vitendo vya ukatili wa kijinsia. Aidha, Wizara hizo pia
zilitoa huduma na kutatua malalamiko kutoka kwa wananchi. Amevishukuru Vyombo
vya Habari kwa kurusha vipindi kwenye redio na TV na kutoa taarifa za
maadhimisho hayo tangu yalipozinduliwa tarehe 3 Desemba, 2023.
Maadhimisho hayo yanaenda
sambamba na maadhimisho ya miaka 75 ya Tamko la Dunia kuhusu haki za binadamu
la mwaka 1948 ambapo Tanzania ni miongoni mwa nchi wanachama wa Umoja wa
Mataifa iliyoridhia mikataba mbalimbali ikiwemo ya haki za binadamu ya Kikanda na Kimataifa.
Comments
Post a Comment