Posts

Showing posts from 2024

WIZARA YAPOKEA MAGARI TISA KATI YA KUMI KURAHISISHA HUDUMA ZA KISHERIA KWA WANANCHI

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akikata utepe kuashiria mapokezi na uzinduzi wa magari tisa kati ya kumi yatakayotumika katika kutoa huduma za Msaada wa Kisheria kwa Wananchi katika maeneo mbalimbali nchini. 20 Desemba, 2024. Mwonekano wa magari tisa kati ya kumi yaliyopokelewa katika Wizara ya Katiba na Sheria kwa ajili ya kurahisisha utekelezaji wa shughuli za utoaji wa msaada wa kisheria kwa wananchi katika maeneo mbalimbali nchini. 20 Desemba, 2024. Watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakiongozwa na Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro wakishangalia na kumkabidhi tuzo ya utendaji bora Katibu Mkuu wa Wizara Bw. Eliakim Maswi mara baada ya Wizara hiyo kushika nafasi ya pili katika Wizara zinazojali maslahi ya Watumishi. 20 Desemba, 2024. xxxxxxxxxxxxxxxxxxx Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damasi Ndumbaro amewataka watumishi wa wizara ya Katiba na Sheria kufanya kazi kwa weledi na ufanisi kutokana na Serikali kuweka mazi...

MSLAC KUTATUA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI KILOSA

Image
  xxxxxxxxxxxxxxxxxx Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amesema Wilaya ya Kilosa imekuwa ikikabiliwa na migogoro mingi ikiwemo ya wakulima na wafugaji na kwamba imekuwa makao makuu ya migogoro ambayo mwarobaini wake ni Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia - Mama Samia legal Aid Campaign. Waziri Ndumbaro amebainisha hayo Desemba 15, mwaka huu wakati akizindua kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia katika kata ya Magomeni Wilayani Kilosa Mkoani humo ikiwa ni siku ya pili baada ya kampeni hiyo kuzinduliwa Kimkoa Disemba 13, 2024. Zaidi, Waziri huyo amesema migogoro inayowakabili wananchi wa Kilosa kumeifanya Wizara ya Uvuvi na Mifugo kuteua Kilosa kuwa makao makuu ya migogoro ya wakulima na wafugaji, hivyo ameitaka timu ya wanasheria wa kampeni hiyo kuandaa ripoti itakayoonesha migogoro iliyotatuliwa na ambayo haijatatuliwa ili ambayo haijatatuliwa ifanyiwe oparesheni maalum ya siku kumi kuhakikisha inaisha. "Na mimi niseme sasa baada ya siku hizi k...

RAIS SAMIA ANATAKA MIGOGORO IFIKIE MWISHO - WAZIRI NDUMBARO

Image
 xxxxxxxxxxxxxxxxx Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia katika Wilaya ya Kilombero Kijiji cha Mkamba, tarehe 14 Desemba, 2024 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amesema kuwa Kampeni hiyo ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ikiwa ni kuonesha mapenzi makubwa aliyonayo kwa Watanzania kwa kuwafikishia huduma za Msaada wa Kisheria bure. Waziri Ndumbaro amesema kuwa, utekelezaji wa Kampeni hiyo utawasaidia Wananchi katika utatuzi wa Changamoto za Kisheria ikiwa ni pamoja na kupeleka huduma za Msaada wa Kisheria karibu na Wananchi. "Utoaji wa Msaada wa Kisheria bure kwa Watanzania ni jambo ambalo halijawahi kutokea tangu Uhuru. Hii inaonesha ni kwa namna gani Rais anawajali Wananchi wake."Alisema Ndumbaro. Aliendelea kusema, "Utekelezaji wa Huduma ya Msaada wa Kisheria ni maelekezo mahususi yaliyotolewa kwa Wizara na Mhe. Rais ambapo aliiagiza Wizara ...

UZINDUZI WA SIKU YA MAADILI NA HAKI ZA BINADAMU

Image
Mgeni Rasmi Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi nya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora akisoma hotuba yake katika kuadhimisha Siku ya Maadili na Haki za Binadamu. Tarehe 5 Novemba, 2024 katika Ukumbi wa Ofisi za Takwimu Dodoma. Kutoka kushoto, Katibu Mkuu wa Katiba na Sheria Bw. Eliakim C. Maswi, katikati ni Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Jaji Mstaafu Mhe. Mathew Mwaimu na aliyepo kulia ni Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Bibi Neema M. Mwakalyelye wakifuatilia maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu. Tarehe 5 Novemba, 2024. Naibu Katibu Mkuu wa Katiba na Sheria Dr. Franklin Rwezimula (kushoto) akiteta jambo na Katibu Mkuu Ikulu Mululi Majula Mahendeka kabla ya kuanza maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu. Tarehe 5 Novemba, 2024. xxxxxxxx Menejimenti ya Wizara ya Katiba na Sheria ikiongozwa na Katibu Mkuu Bwana Eliakim C. Maswi imeshiriki Uzinduzi Wa Siku ya Maadili na Hak...

UONGOZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU YAKUTANA NA VIONGOZI WA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

Image
Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu Mhe. Jaji Imani Aboud akimkabidhi zawadi Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi mara baada ya kukutana na Uongozi wa Mahakama hiyo, tarehe 04, Desemba 2024 Mtumba, jijini Dodoma. Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu Mhe. Jaji Imani Aboud akiteta jambo na Katibu Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Eliakim Maswi akiwa pamoja na Naibu Katibu Dkt. Franklin Rwezimula mara baada ya kukamilika kwa mazungumzo baina ya Viongozi hao tarehe 04 Desemba, 2024 katika ukumbi wa Wizara Mtumba, jijini Dodoma. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu Mhe. Jaji Imani Aboud (wa kwanza kulia kwa Waziri) pamoja na Viongozi wa Mahakama hiyo na Viongozi wa Wizara mara baada ya kukamilika kwa mazungumzo baina ya Viongozi hao, tarehe 04 Desemba, 2024 katika ukumbi wa Wizara Mtumba, jijini Dod...

TUME YA TEC YAKUTANA NA KABUDI NA KATAMBI

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi   akifafanua jambo katika kikao hicho pembeni yaka ni Mhe. Patrobas Katambi, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu walipokutana na Tume ya TEC Mtumba Dodoma leo 07/11/2024. Baadhi ya wawakilishi wa Tume ya Kimisionari ya Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki (TEC) wakiongozwa na Mwenyekiti wa Tume hiyo Askofu Damian Dallu (Wa kwanza Kuala) wakifuatilia mazungumzo hayo. Mhe. Patrobas Katambi, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu akichangia hoja katika mazungumzo hayo. Jopo la wawakilishi wa Tume ya Kimisionari ya Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki (TEC) kwenye picha ya pamoja na Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi na Mhe. Patrobas Katambi, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu pamoja na wajumbe wa menejimenti ya Wizara ya Katiba na Sheria. Mwenyekiti...
Image
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Eliakim Maswi akiongoza Kikao Kazi kilichowakutanisha Wizara, Baraza la Uongozi la Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) na  Kitengo cha Kuzuia Utakatishaji wa Fedha Haramu, tarehe 31 Oktoba, 2024 ofisi za Wizara Mtumba, Dodoma. xxxxxxxxx Wito huo umetolewa na Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Eliakim Maswi katika kikao kazi kilichowakutanisha Wizara, Baraza la Uongozi la Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) na  Kitengo cha Kuzuia Utakatishaji wa Fedha Haramu  kwa lengo la kujengeana uwezo wa utekelezaji wa masharti ya Sheria ya Udhibiti wa Fedha Haramu, kikao kilichofanyika tarehe 31 Oktoba, 2024 katika ukumbi wa Wizara Mtumba, jijini Dodoma. Kwa mujibu wa Katibu Mkuu, kulijenga Taifa la Tanzania kunahitaji ushirikiano baina ya Taasisi mbalimbali na ni jambo lisilokwepeka  hivyo ni vyema kukaa kwa pamoja  ili kujua majukumu ya kila mmoja katika kutafuta mustakabali wa kuzuia biashara hiyo.  Maswi amesema wap...

"MAJAJI NA WAENDESHA MASHTAKA WAJENGEWE UWEZO KUENDESHA MASHAURI DHIDI YA BIASHARA HARAMU YA BINADAMU" - MASWI

Image
  Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Eliakim Maswi (katikati) akizungumza katika kikao kilichowakutanisha wataalam kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na ujumbe kutoka Nchini Marekani wanaohusika na mapambano na ufuatiliaji dhidi ya biashara ya usafirishaji haramu wa Binadamu. Tarehe 30 Oktoba, 2024 ofisi za Wizara Mtumba, Dodoma. Ofisa kutoka Ofisi inayoshughulika utokomezaji na ufuatiliaji wa biashara ya usafirishaji haramu wa Binadamu kutoka nchini Marekani Bw. Adam Blakeman amesema kuwa  Nchi ya Tanzania ni miongoni mwa Nchi zilizopiga  hatua kubwa katika mapambano dhidi ya biashara hiyo ukilinganisha na Nchi nyingine barani Afrika. xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Eliakim Maswi amesema Nchi ya Tanzania imefanya jitihada mahususi katika kupambana na usafirishaji haramu wa Binadamu ikiwemo marekebisho ya S...

BODI YA KITAIFA YA USHAURI YA MSAADA WA KISHERIA YATEMBELEA WASAIDIZI WA KISHERIA IRINGA

Image
Mwenyekiti wa Bodi ya Kitaifa ya Ushauri ya Msaada wa Kisheria Bwana Saulo Malauri akifafanua jambo ikiwa ni sehemu ya ziara ya bodi hiyo kutembelea mashirika wa wasaidizi wa kisheria Mkoani Iringa, 24/10/2024. Mratibu wa Shirika la Kilolo Paralegal Unit  akitoa Maelezo ya utekelezaji kwa Bodi ya Kitaifa ya Ushauri ya Msaada wa Kisheria ilipofika katika ofisi za shirika zilizopo Ilula wilayanii Kilolo tarehe 24/10/2024. Wajumbe wa Bodi na wasaidizi wa kisheria wa Kilolo Paralega Unit wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumaliza mazungumzo patika shirika hilo. Tarehe 24/10/2024. xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx Na Lusajo Mwakabuku – WyKS Iringa Bodi ya Kitaifa ya Ushauri ya Msaada wa Kisheria ikiwa katika kikao kazi cha Kumi kinachofanyika kwa siku mbili Mkoani Iringa imefanya ziara ya kuwatembelea watoa huduma za msaada wa kisheria waliopo Iringa Mjini na Wilaya ya Kilolo kwa lengo la kukagua utekelezaji wa majukumu yao na kubaini changamoto zao. Bodi hiyo ...

HAKI ZA BINADAMU ZIZINGATIE MAKUNDI YA WANAWAKE NA WANAUME - SAGINI

Image
  Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini akihutubia wakati akifungua kikao kazi cha kuandaa taarifa ya Nchi ya utekelezaji wa Mkataba wa Afrika   wa Haki za Binadamu na Watu pamoja na Itifaki ya Maputo ya Haki za Wanawake Afrika, Oktoba 23, 2024 Morogoro. Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini kwenye picha ya pamoja na washiriki wa kikao kazi cha kuandaa taarifa ya Nchi ya utekelezaji wa Mkataba wa Afrika  wa Haki za Binadamu na Watu pamoja na Itifaki ya Maputo ya Haki za Wanawake Afrika, Oktoba 23, 2024 Morogoro. xxxxxxxxxxxxxxxxx Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini (Mb) ameitaka timu ya Wataalam kutoka Tanzania Bara na Zanzibar inayoshiriki katika kuandaa na kukamilisha rasimu ya taarifa ya Nchi kuhakikisha taarifa zinazoandaliwa katika kuimarisha Haki za Binadamu zinajumuisha jinsia ya Kike na Kiume na kuepuka kuimarisha kundi moja pekee kwani makundi  haya yanategemeana. Naibu Waziri Sagini ameyasema hayo Oktoba 23, 20...

KATIBA NA SHERIA YAWAKUTANISHA WADAU KUJADILI UTEKELEZAJI WA MIKATABA YA HAKI ZA BINADAMU

Image
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Haki za Binadamu Bw. Richard Kilanga  akizungumza katika kikao kazi kilichowakutanisha wadau mbalimbali kwa lengo la  kukamilisha taarifa ya Nchi ya kufuatilia utekelezaji wa Mkataba wa Kimataifa na Kikanda wa Haki za Binadamu na Watu pamoja na Mkataba wa Haki za Wanawake Barani Afrika  (Itifaki ya Maputo) tarehe 22 Oktoba, 2024 mjini Morogoro. Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Haki za Binadamu Bi. Beatrice Mpembo  akizungumza katika kikao kazi kilichowakutanisha wadau mbalimbali kwa lengo la  kukamilisha taarifa ya Nchi ya kufuatilia utekelezaji wa Mkataba wa Kimataifa na Kikanda wa Haki za Binadamu na Watu pamoja na Mkataba wa Haki za Wanawake Barani Afrika  (Itifaki ya Maputo) 22Oktoba, 2024 mjini Morogoro. Baadhi ya Washiriki wakiwa katika kazi za vikundi  wakipitia taarifa mbalimbali za utekelezaji wa Mkataba wa Kimataifa na Kikanda wa Haki za Binadamu na Watu pamoja na Mkataba wa Haki za Wanawake barani Afrika...

WAZAZI ANDIKENI WOSIA KUEPUSHA MIGOGORO YA MIRATHI – SAGINI

Image
  Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini (Mb) alipokuwa akifungua Mafunzo kuhusu Huduma za Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) kwa Makatibu Tawala, na Maofisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri za Mikoa ya Mara, Mwanza, Kagera, Geita, Simiyu na Shinyanga. Oktoba 21, 2024 Butiama. Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini (Mb) kwenye picha ya pamoja na baadhi ya washiriki kwenye Mafunzo kuhusu Huduma za Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) kwa Makatibu Tawala, na Maofisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri za Mikoa ya Mara, Mwanza, Kagera, Geita, Simiyu na Shinyanga. Oktoba 21, 2024 Butiama. xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini (Mb) amesema kuwa chanzo kikuu cha matatizo ya mirathi ni wazazi kutoandika wosia na kusabisha wajane na warithi halali kudhulumiwa mali baada ya mzazi mmoja hasa baba kufariki. Mhe. Sagini ameyasema hayo leo Oktoba 21, 2024 wakati alipokuwa akifungua Mafunzo kuhusu Huduma za W...

SERIKALI INA DHAMIRA THABITI YA KUWALINDA WATOTO DHIDI YA UKATILI

Image
  Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Franklin Rwezimula na Wakili Bonifasi K. Mwabukusi – rais wa TLS wakishiriki matembezi ya amani dhidi ya vitendo vya ukatili na mauaji kwa watoto tarehe 18/10/2024 jijini Dar es salaam. Naibu Katibu Mkuu wa Katiba na Sheria Dkt. Franklin Rwezimula na Wakili Bonifasi K. Mwabukusi – rais wa TLS pamoja na Mawakili wakiwasili katika viwanja vya Mnazi Mmoja baada ya matembezi ya amani dhidi ya vitendo vya ukatili na mauaji kwa watoto tarehe 18/10/2024 jijini Dar es salaam. Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Katiba na Ufuatiliaji Haki kutoka Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Beatrice Mpembo akipokea tuzo ya cheti  cha udhamini kwa niaba ya Wizara ya Katiba na Sheria kwenye matembezi ya amani dhidi ya vitendo vya ukatili na mauaji kwa watoto tarehe 18/10/2024 jijini Dar es salaam. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Franklin Rwezimula akiambatana na Wakili Bonifasi K. Mwabukusi – rai...

KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA KUFANYIKA MIKOA MINNE KWA PAMOJA

Image
  Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Msaada wa Kisheria Bi. Ester Msambazi akifungua mafunzo kwa Viongozi wa Makundi (Team Leaders) katika ukumbi wa Hotel ya Edema Morogoro mjini tarehe 17/10/2024. Wakili wa Serikali kutoka Katiba na Sheria Bw. Candid Nasua akifanya wasilisho katika mafunzo kwa Viongozi wa Makundi (Team Leaders) yatakayotoa msaada wa kisheria katika kampeni ya MSLAC katika ukumbi wa Hotel ya Edema Morogoro mjini tarehe 17/10/2024. Baadhi ya washiriki wa mafunzo kwa Viongozi wa Makundi (Team Leaders) yatakayotoa msaada wa kisheria katika kampeni ya MSLAC wakifuatilia wasilisho katika ukumbi wa Hotel ya Edema Morogoro mjini tarehe 17/10/2024. xxxxxxxxxxxxxxxxxxxx Wizara ya Katiba na Sheria ipo katika hatua za mwisho za maandalizi ya kuendeleza utekelezaji wa kampeni ya msaada wa kisheria katika Mikoa Minne ambayo ni Mororgoro, Iringa, Songwe na Mara. Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Msaada wa Kisheria Bi. Ester Msambazi wakati akimwakili...

WAZIRI KABUDI APOKEA TAARIFA NANE ZA MAPITIO YA SHERIA

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi akiongea wakati wa hafla ya kukabidhiwa taarifa nane za tafiti za mapitio ya Sheria zilizofanywa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2023/2024 kutoka Tume ya Kurekebisha Sheria Nchini (LRCT), 16 Oktoba, 2024. Mtumba jijini Dodoma. Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Nchini (LRCT) Mhe. Jaji Winfrida Korosso akiongea wakati wa hafla ya kukabidhi taarifa nane za tafiti za mapitio ya Sheria zilizofanywa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2023/2024 na Tume hiyo, 16 Oktoba, 2024. Mtumba jijini Dodoma. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi akipokea taarifa nane za tafiti za mapitio ya Sheria  zilizofanywa kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2023/2024 na Tume ya Kurekebisha Sheria Nchini (LRCT) kutoka kwa Mwenyekiti  wa Tume hiyo Mhe. Jaji Winfrida  Korosso, 16 Oktoba, 2024. Mtumba jijini Dodoma. xxxxxxxxxxxxxxxxxxxx Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba ...