BALOZI DKT. CHANA AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA UINGEREZA
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akiongea kwenye kikao na Balozi wa Uingereza, tarehe 31 Januari, 2024 Ofisi za Bunge, Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana na Balozi wa Uingereza nchini Mhe. David Concar, tarehe 31 Januari, 2024 Ofisi za Bunge, Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana na Balozi wa Uingereza nchini Mhe. David Concar, kwenye picha ya pamoja na walishiriki katika kikao hicho, tarehe 31 Januari, 2024 Ofisi za Bunge, Dodoma.
Na William Mabusi – WKS Dodoma
Waziri wa Katiba na Sheria
Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa
Uingereza nchini Tanzania, Mhe. Balozi David Concar tarehe 31 Januari, 2024
Ofisi za Bunge Dodoma.
Mazungumzo hayo yalilenga
kuweka vipaumbele vya mradi mpya wa BSAAT unaotarajiwa kuanza baadaye mwaka huu
baada ya mradi unaoendelea kuisha muda wake. Katika kikao hicho Dkt. Chana
kupitia Ubalozi wa Uingereza nchini, ameishukuru Serikali ya Uingereza kwa
ufadhili wa mradi huo ambao pamoja na masuala mengine umesaidia kuleta mapinduzi
makubwa katika kupambana na rushwa nchini, utungaji wa Kanuni za Kuwalinda
Watoa Taarifa na Mashahidi, 2023, ujenzi wa Kituo cha kupokea taarifa na
malalamiko.
Dkt. Chana ametaja maeneo ya
kipaumbele kwenye mradi ujao kuwa ni pamoja na kuimarisha ofisi na vitendea
kazi kwenye Wizara na Taasisi za haki jinai, kufanya marekebisho ya Sheria ya
Kuwalinda Watoa Taarifa na Mashahidi (Whistle Blower Act, 2015), kujenga uwezo
kwenye uandaaji wa miswada ya kisheria na mikataba hususan ya ulinzi wa
maliasilia za nchi, kuwajengea uwezo Waendesha Mashtaka na Wachunguzi wa makosa
ya jinai ili kupambana na mbinu mpya za uhalifu.
Akiongea katika kikao hicho Mhe. Balozi Concar amesema Serikali ya Uingereza itaendelea na ufadhili wa mradi wa BSAAT kuunga jitihada za Serikali katika kupambana na rushwa, Ukatili wa kijinsia na watoto na utekelezaji wa mapendekezo ya Tume ya Haki Jinai.
Comments
Post a Comment