MAADHIMISHO YA WIKI YA SHERIA YAANZA VIWANJA VYA NYERERE DODOMA
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma Mhe. Dkt. Juliana
Masabo akisaini kitabu cha mahudhurio kwenye Banda la Wizara kwenye maadhimisho
ya Wiki ya Sheria, tarehe 24 Januari, 2024 viwanja vya Nyerere Square
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Na William Mabusi –
WKS Dodoma
Madhimisho ya Wiki ya Sheria ambayo huandaliwa na Mahakama
ya Tanzania kila mwaka yameanza leo tarehe 24 Januari, 2024 kwenye viwanja vya
Nyerere Square, Jijini Dodoma ambapo Wizara ya Katiba na Sheria inashiriki.
Maadhimisho hayo ya siku tisa yaliyobeba kauli mbiu ”Umuhimu
wa Dhana ya Haki kwa Ustawi wa Taifa: Nafasi ya Mahakama na Wadau katika
Kuboresha Mfumo Jumuishi wa Haki Jinai” yatazinduliwa rasmi tarehe 27 Januari,
2024 na kufungwa rasmi tarehe 1 Februari, 2024. Wakati wote wa maadhimisho hayo
Wizara itakuwa inatoa elimu ya sheria na huduma ya msaada wa kisheria.
Comments
Post a Comment