TUWASHIRIKISHE WANANCHI ULINZI WA UTAJIRI ASILIA



 

Mgeni Rasmi Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali waliofika katika mafunzo hayo ya kujengeana uwezo juu ya mali asilia, Januari 18, 2024 Jijini
 Dar es Salaam.


Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Hazara Chana akizungumza na Makatibu Wakuu, Wakuu wa Taasisi na Wadau mbalimbali wa Sekta ya Utajiri na Mali Asili za nchi wakati wa ufunguzi wa mkutano wa siku mbili wa majadiliano, Januari 18, 2024 Jijini Dar es salaam.

Naibu Katibu Mkuu wa Katiba na Sheria Dr. Khatibu Kazungu akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Waziri wa katiba na Sheria kutoa hotuba yake, Januari 18, 2024 Jijini Dar es Salaam.

XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

Na Lusajo Mwakabuku - WKS Dar es Salaam

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Hazara Chana amewataka Viongozi wa umma wenye jukumu la kusimamia Utajiri Asili na Mali Asilia za nchi kuwashirikisha wananchi katika kulinda rasilimali hizo ili kuhakikisha zinalinufaisha taifa na wananchi kwa ujumla wake.

Dkt. Chana amesema hayo Januari 18, 2024 jijini Dar es salaam wakati wa ufunguzi wa mkutano wa majadiliano uliowakutanisha Makatibu Wakuu, Wakuu wa Taasisi na Wadau mbalimbali wa Sekta ya Utajiri na Mali Asili za nchi kwa lengo la kuwajengea uelewa wa kusimamia na kufanya uangalizi wa utajiri asili na mali asilia za nchi.

Aidha, Waziri Dkt. Chana amesema mafunzo hayo yatasaidia kuongeza maarifa ya kuwawezesha watumishi hao kusimamia vyema rasilimali za nchi ili kuvutia uwekezaji utakaoleta manufaa kwa taifa na wananchi ambapo pia amewataka watumishi hao kuja na mikakati na kuishauri Serikali kuhusu utajiri asili na mali asilia za nchi.

"Dhamira hii inaenda sambamba na matakwa ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi CCM ambayo inasisitiza kusimamia uwekezaji wa sheria za kulinda rasilimali za taifa na kuboresha sera na sheria zinazohusu ulinzi, uendelezaji, uwekezaji katika rasilimali za taifa hususan kusimamia utekelezaji wa sheria za kuwezesha majadiliano kwenye mikataba ya uwekezaji katika utajiri asili na mali asilia za nchi." Alisema Waziri Dkt. Pindi Chana

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kitengo cha Uangalizi wa Utajiri na Mali Asilia za Nchi Kamishna wa Polisi Neema Mwanga amebainisha kuwa ipo haja ya kuweka misingi imara ya kisheria na usimamizi wa rasilimali asilia ambazo zitasaidia kuvutia wawekezaji.

"Sheria hizi zinatutaka tusiingie mikataba isipokuwa tu pale ambapo tunahakikisha wananchi watafaidika, kuna njia nyingi ambazo wananchi wanaweza kunufaika na rasilimali hizi, wengine kwa kupata ajira na wengine watafaidika kwa kuingia mikataba midogo midogo kama vile usambazaji wa vyakula katika miradi inayoendeshwa"



Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA