WAZIRI CHANA AFANYA KIKAO NA VIONGOZI WA TAASISI YA USULUHISHI TANZANIA
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe.Balozi Dkt Pindi Chana akitoa
ufafanuzi kwenye kikiao na viongozi wa Taasisi ya
usuruhishi (Tanzania Institute of Arbitrators)
kilichofanyika leo tarehe 29 Janauri 2024 jijini Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe.Balozi Dkt Pindi Chana akipokea vitabu kutoka kwa Makamu wa Rais wa Taasisi ya Usuruhishi Ndg, Anderickson Njunwa kwenye kikiao kilichofanyika leo tarehe 29 Janauri 2024 jijini Dodoma.
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Na, George Mwakyembe
- WKS Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe.
Balozi Dkt. Pindi Chana amekutana na kufanya kikao na viongozi kutoka Taasisi
ya Usuluhishi wa migogoro ya Kibiashara kwa Njia Mbadala - TIARB (Tanzania
Insitute of Arbitrators) na kujadili masuala mbalimbali ya namna ya kutatua
migogoro kwa njia ya mapatano badala ya kwenda mahakamani.
Akizungumza katika kikao hicho
kilichofanyika leo tarehe 29 Januari 2024 jijini Dodoma, Mhe Balozi Chana
amesema ni vyema taasisi hiyo ikaweka nguvu kubwa katika kujitangaza (Branding) ili wananchi
waweze kujua na kutambua umuhimu wa kutatua migogoro kwa njia ya amani.
“Kutatua migogoro nje ya Mahakama
kunajenga ushirikiano kwenye jamii zetu lakini pia kunaondoa chuki baina ya
wagombanao, ni gharama nafuu pamoja na inachukua muda mfupi. Hivyo ni lazima
kuwaeleza na kuwaeleimisha watanzania kutumia njia hizi za utatuzi wa migogoro
badala ya kukimbilia mahakamani” Alisema Waziri Chana.
Naye, Makamu wa Rais wa Taasisi
hiyo Ndg, Anderickson Njunwa alieleza kuwa wao kama taasisi wamejipanga kuhakikisha
watoa elimu kwa watanzania pamoja na semina mbalimbali za namna ya kutatua
migogoro kwa njia ya upatanishi na mashauriano
ili kupunguza kesi mahakamani lakini pia kujenga upendo na ushirikiano
katika jamii zetu.
Akiongelea mikakati mbalimbali
ambayo taasisi hiyo inaendelea kuitekeleza, Bwana Njunwa alisema kwa mwaka huu
tayari wameweka mkakati wa kuendesha semina na mikutano mbalimbali kwa lengo la
kuwajengea uwezo wasuruhishi pamoja na watatuzi wa mogogoro.
Taasisi ya Usuluhishi Tanzania
(TIArb) ilisajiliwa Desemba 1999 na Msajili wa Vyama kwa Cheti cha Usajili
Namba 8833. Kazi kubwa ya TIArb ni kukuza na kuwezesha utatuzi wa migogoro ya
kibiashara nchini Tanzania. Kabla ya kuanzishwa kwake, Baraza la Kitaifa la
Ujenzi (NCC) lilikuwa likichukua jukumu kama hilo kwa migogoro inayohusiana na
ujenzi pekee.
Comments
Post a Comment