BAJETI ZIZINGATIE UTEKELEZAJI WA 4R ZA MHE. RAIS – DKT. CHANA
Katibu Mtendaji wa Tume ya kurekebisha Sheria Bw. George Mandepo akitoa wasilisho fupi la maoteo ya bajeti ya Taasisi yake kwa mwaka wa fedha 2024/25, tarehe 06 Februari, 2024 Ofisi za Bunge Dodoma.
Kabidhi Wasii Mkuu ofisi ya RITA Bw. Frank Kanyusi akitoa wasilisho fupi la maoteo ya bajeti ya Taasisi yake kwa mwaka wa fedha 2024/25, tarehe 06 Februari, 2024 Ofisi za Bunge Dodoma.
Na William Mabusi – WKS Dodoma
Waziri wa Katiba na Sheria
Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana ameziagiza Taasisi za Wizara hiyo kuhakikisha
zinazingatia pamoja na mambo mengine ya maendeleo lakini pia utekelezaji wa R4
za Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Dkt. Chana ametoa agizo hilo
wakati alipokutana na Wakuu wa Taasisi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Wizara,
Wakurugenzi kutoka Wizarani na kupitishwa kwenye maoteo ya Bajeti ya mwaka
fedha 2024/25 kwa Taasisi hizo tarehe 06 Februari, 2024 kwenye ofisi za Bunge
Jijini Dodoma.
”Katika kipindi hiki cha
kukamilisha maandalizi ya bajeti kwa mwaka wa fedha 2024/25 kila Taasisi na
Mkuu wa Taasisi atwambie namna ambavyo amejipanga kuzitekeleza zile R4 za Mhe.
Rais. Pangeni kufanya mageuzi na maboresho makubwa kwenye matumizi ya TEHAMA, Kufanya
tathmini na mapitio ya sheria mbalimbali, Kuongeza visibility kwa maana
ya kutangaza Taasisi zenu na Kuendelea kutoa elimu kwa umma, Kuwajengea uwezo
watumishi.” Alisema Dkt. Chana huku akihimiza pia Taasisi hizo kuongeza
mashirikiano na Wadau wa Maendeleo kwenye ufadhili wa miradi ya maendeleo.
Comments
Post a Comment