IGUNGA KUPATA JENGO JIPYA LA MAHAKAMA YA WILAYA
Na
William Mabusi – WKS Dodoma
Waziri
wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amesema Serikali imepanga
kujenga jengo la Mahakama ya Wilaya ya Igunga katika mwaka wa fedha 2024/25.
Dkt.
Chana amesema hayo tarehe 06 Februari, 2024 Bungeni alipokuwa anajibu swali la
Mbunge wa Igunga Mhe. Nicholaus George
Ngassa aliyetaka kujua lini Serikali itajenga jengo la Mahakama ya Wilaya ya
Igunga.
“Igunga
ni moja ya Wilaya ambazo hazina jengo la Mahakama ya Wilaya kwa muda mrefu. Kwa
sasa Mahakama ya Wilaya inafanya kazi ndani ya jengo moja na Mahakama ya Mwanzo
Igunga mjini, jengo ambalo lilijengwa kwa ajili ya Mahakama ya Mwanzo. Kwa
kuzingatia Mpango wa ujenzi wa Mahakama, jengo la Mahakama ya Wilaya ya Igunga
linatarajiwa kujengwa katika Bajeti ya Mwaka 2024-25.” Amesema.
Comments
Post a Comment