DKT. CHANA AMPOKEA JUMANNE SAGINI
Waziri
wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akimkabidhi ua la ukaribisho
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini alipowasili Ofisi ya
Wakili Mkuu wa Serikali mara baada ya hafla ya uapisho iliofanyika Ikulu Jijini
Dar es Salaam tarehe 04 Aprili, 2024. Anayeshuhudia katikati ni Katibu Mkuu wa
Wizara hiyo, Bi. Mary Makondo.
Waziri
wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akizungumza na viongozi wa
Wizara na Taasisi zilizoko chini ya Wizara hiyo mara baada ya kumkaribisha na
kumpokea Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Jumanne Sagini katika mapokezi
yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali Jijini Dar es
Salaam baada ya kuapishwa Ikulu, tarehe 04 Aprili, 2024.
Naibu Waziri wa Katiba na
Sheria Mhe. Jumanne Sagini akizungumza na Viongozi wa Wizara na Taasisi zilizo
chini ya Wizara hiyo mara baada ya kuapishwa Ikulu Jijini Dar es Salaam. Kulia
kwake ni Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana. 04
Aprili, 2024.
Katibu Mkuu wa Wizara ya
Katiba na Sheria, Bi. Mary Makondo akizungumza na Viongozi wa Wizara na Taasisi
zilizo chini ya Wizara hiyo wakati akimkaribisha Waziri wa Wizara hiyo, Mhe.
Balozi Dkt. Pindi Chana amkaribishe Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Jumanne
Sagini ili azungumze na viongozi hao. 04 Aprili, 2024.
Naibu Waziri wa Katiba na
Sheria Mhe. Jumanne Sagini akisaini kitabu cha wageni alipowasili Ofisi ya
Wakili Mkuu wa Serikali mara baada ya kuapishwa Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Anayeshuhudia ni Kaimu Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Mark Mulwambo.
04 Aprili, 2024.
Viongozi wa Wizara na Taasisi
za Wizara ya Katiba na Sheria wakimsikiliza Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Balozi
Pindi Chana (hayupo pichani) baada ya hafla ya kuapishwa Ikulu kwa Naibu Waziri
wa Wizara hiyo, Mhe. Jumanne Sagini Jijini Dar es Salaam. 04
Aprili, 2024.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Jumanne Sagini akisalimiana na watumishi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali alipowasili Ofisini hapo mara baada ya kuapishwa Ikulu Jijini Dar es Salaam. 04 Aprili, 2024.
Comments
Post a Comment