MASHAURI 705 YAOKOA TRILIONI 3.4 FEDHA ZA SERIKALI
Naibu Waziri wa Katiba na
Sheria Mhe. Jumanne Sagini akihutubia wakati wa ufunguzi wa mkutano wa pili wa
Baraza la Pili la Wafanyakazi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, Aprili 19,
2024 Mkoani Morogoro.
Wakili Mkuu wa Serikali Dkt. Boniphace Luhende na Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi akisoma hotuba wakati wa ufunguzi wa mkutano wa pili wa Baraza la pili la Wafanyakazi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, Aprili 19, 2024 Mkoani Morogoro.
Kaimu Naibu Wakili Mkuu wa Serikali Ndg. Mark Mulwambo akizungumza wakati wa ufunguzi wa Baraza la Wafanyakazi, Aprili 19, 2024 Mkoani Morogoro.
Naibu Waziri wa Katiba
na Sheria Mhe. Jumanne Sagini (katikati) akiongoza zoezi la kuimba wimbo wa
mshikamano ikiwa ni ishara rasmi ya kuanza kwa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi
wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali. Pamoja naye ni Wakili Mkuu wa Serikali
Dkt. Boniphace Luhende (wa kwanza kulia kwake), Kaimu Naibu Wakili Mkuu wa
Serikali Ndg. Mark Mulwambo (wa pili kulia) pamoja na
viongozi wengine wa Baraza hilo. Aprili 19, 2024 Mkoani Morogoro.
Baadhi ya Watumishi wa Ofisi
ya Wakili Mkuu wa Serikali wakifuatilia hotuba ya Mgeni Rasmi ambaye ni Naibu
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini katika ufunguzi wa mkutano
wa pili wa Baraza la pili la Wafanyakazi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, Aprili
19, 2024 Mkoani Morogoro.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini (kushoto) akipokea zawadi kutoka kwa Wakili Mkuu wa Serikali Dkt. Boniphace Luhende (kulia) mara baada ya kukamilika kwa kufungua mkutano wa pili wa Baraza la pili la Wafanyakazi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, Aprili 19, 2024 Mkoani Morogoro.
Naibu Waziri wa Katiba na
Sheria Mhe. Jumanne Sagini (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi
wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali mara baada ya kufungua mkutano wa
pili wa Baraza la pili la Wafanyakazi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, Aprili
19, 2024 Mkoani Morogoro.
xxxxxxxxxxxxxxxxx
Na Yasinta Kisima – WKS Morogoro
Naibu Waziri wa Katiba na
Sheria Mhe. Jumanne Sagini ameipongeza Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali katika
kusimamia na kushinda Mashauri 705 yenye madai ya fedha na kuipelekea
Serikali kuokoa zaidi ya Shilingi Trilioni 3.47 kwa kipindi cha Julai 2023 hadi
Aprili 2024.
Mhe. Sagini ameyasema hayo
Aprili 19, 2024 wakati akifungua kikao cha pili cha Baraza pili la
Wafanyakazi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali kwa mwaka wa fedha 2023/2024
katika ukumbi wa mikutano wa NSSF, Mkoani Morogoro.
"Ofisi ya Wakili Mkuu wa
Serikali imeonesha uzalendo na weledi katika kuhahikisha Serikali inashinda
katika Mashauri na usuluhishi ndani na nje ya nchi. Fedha ambazo zimeokelewa ni
mchango mkubwa katika kuisaidia Serikali kwenye utekelezaji wa miradi mikubwa
ya maendeleo. Niwapongeze kwa hatua hii na niwasihi tuendelee kulipigania
Taifa." Alisema Mhe. Sagini.
Aliendele kusema
"Tunaishukuru sana Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt.
Samia Suluhu Hassan kwa jinsi inavyoiwezesha Ofisi hii. Ongezeko la bajeti
kutoka Shilingi Bilioni 17 zilizotengwa mwaka 2023/2024 hadi kufikia ukomo wa
Shilingi Bilioni 20.7 kwa mwaka 2024/2025 ongezeko la takribani shilingi
Bilioni 3.6 ni ishara kubwa kwamba Mhe. Rais anatambua mchango mkubwa wa Ofisi
hii katika kuiwakilisha Serikali na Taasisi zake katika mashauri ya madai na
usuluhishi"
Katika hatua nyingine Mhe.
Sagini amesema kupitia mikakati ya Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali katika
kushughulikia mashauri ya ardhi Wizara ya Katiba na Sheria itaendelea
kushirikiana na Wizara ya Ardhi ili kuendelea na jitihada za kupunguza migogoro
ya ardhi kwa kuyashughulikia mapema kabla ya kuwasilishwa Mahakamani au
katika mabaraza ya ardhi.
Kwa upande wake Wakili Mkuu wa
Serikali Dkt. Boniphace Luhende amesema kuwa Ofisi imeendelea kuwajengea
uwezo Watumishi kwa kuwapatia mafunzo ya muda mrefu na muda mfupi ikiwemo
mafunzo ya kiubobevu katika maeneo maalumu ambapo kwa kipindi cha Julai 2023,
hadi Aprili 2024 jumla ya Watumishi 11 wamepatiwa ufadhili wa mafunzo ya muda
mrefu na watumishi 56 walipatiwa mafunzo ya muda mfupi ndani na nje ya nchi.
Aidha, Dkt. Luhende amesema
upo uhitaji mkubwa wa Mawakili wenye ubobevu katika maeneo ya gesi, mafuta, uwekezaji,
anga, madini, uchumi wa bluu, TEHAMA ili kuiwezesha Ofisi hiyo kufanya vizuri
zaidi katika maeneo hayo ya kimkakati.
Awali akiwasilisha agenda kuu ya kikao hicho, Kaimu Naibu Wakili Mkuu wa Serikali Ndg. Mark. Mulwambo amesema kuwa kikao hicho kinalenga kupitia na kujadili makadirio ya mpango na Bajeti kwa mwaka wa fedha 2024/2025, ambapo makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka huo ni Shilingi 20,750,720,000. Ofisi ikitaraji kutumia Shilingi Bilioni 4.3 na matumizi mengineyo yakitarajiwa kuwa Shilingi Bilioni 16.4.
Ikumbukwe kuwa, Mabaraza ya
Wafanyakazi mahala pa kazi ni nyenzo muhimu katika kuboresha utendaji na
ufanisi wa utekelezaji wa majukumu kwa Wafanyakazi.
Comments
Post a Comment