UKATILI WOWOTE WANAOFANYIWA WATOTO UTOLEWE TAARIFA – DKT. CHANA
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Khatibu Kazungu akitoa salaam na kumkaribisha Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana kuhutubia Kikao cha Tatu cha Jukwaa la Haki Mtoto, 05 Aprili, 2024 Jijini Arusha.
Sehemu ya Washiriki kwenye Kikao cha Tatu cha Jukwaa la
Haki Mtoto, wakisikiliza hotuba ya Mgeni Rasmi Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi
Dkt. Pindi Chana. 05 Aprili, 2024 Jijini Arusha.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Na Lusajo Mwakabuku – WKS Arusha
Waziri wa Katiba na Sheria
Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amewataka watanzania hususan Vyombo vya Habari
kuongeza juhudi katika kuwalinda Watoto kwa kutoa taarifa za ukatili
unaofanyika dhidi yao ili hatua za
kisheria ziweze kuchukuliwa.
Mhe. Chana ameyasema hayo leo
tarehe 05 Aprili, 2024 wakati akihutubia Kikao cha Tatu cha Jukwaa la Haki
Mtoto kilichofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Four Points Jijini Arusha huku
akiwataka washiriki kuongeza ushirikiano baina yao na Serikali katika kuhakikisha
haki kwa watoto inapatikana.
Comments
Post a Comment