WAZIRI PINDI CHANA AKUTANA NA MENEJIMENTI YA RITA

Kabidhi Wasii Mkuu na Afisa Mtendaji Mkuu wa RITA Ndg. Frank Kanyusi Frank akitoa neno la utangulizi kwa Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini kabla ya kumkaribisha Kaimu Meneja wa Mipango Ufuatiliaji na Tathmini Bw. Ernest Mbuna kuwasilisha Taarifa ya majukumu ya RITA, Aprili 23, 2024 ofisi za Wizara Mtumba.

Kaimu Meneja wa Mipango Ufuatiliaji na Tathmini Bw. Ernest Mbuna kutoka RITA akiwasilisha Taarifa ya majukumu ya RITA kwa Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini, Aprili 23, 2024 ofisi za Wizara Mtumba.

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akiongoza kikao ambapo yeye na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini walikutana na Menejimenti ya RITA, Aprili 23, 2024 ofisi za Wizara Mtumba.



 

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA