BUNGE LAIDHINISHA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akiwasili Bungeni, mkononi ameshika mkoba uliobeba Bajeti ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2024/25 Aprili 29, 2024.

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akisoma hotuba ya bajeti ya mwaka wa fedha 2024/25 Aprili 29, 2024 Bungeni Dodoma.


Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo (kushoto) akiteta jambo na Mwandishi Mkuu wa Sheria Bw. Onorius Njole, wengine katika picha ni Dkt. Boniphace Luhende Wakili Mkuu wa Serikali na Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Jaji Mtaafu Mhe. Mathew Mwaimu wakati wakisubiri kusomwa kwa bajeti ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2024/25 Aprili 29, 2024.


Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (katikati), Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini (kushoto) na Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo kwenye picha ya pamoja baada ya Bunge kupitisha bajeti ya Wizara ya mwaka wa fedha 2024/25, Aprili 29, 2024.

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini pamoja na viongozi wengine wakiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa Wizara na Taasisi zake waliohudhuria kikao cha Bunge, Aprili 29, baada ya Bunge kupitisha bajeti ya Wizara ya mwaka wa fedha 2024/25.

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Jaji Dkt. Eliezer Feleshi, Katibu Mkuu Bi. Mary Makondo kwenye picha ya pamoja na Wakurugenzi waliohudhuria kikao cha Bunge, Aprili 29, baada ya Bunge kupitisha bajeti ya Wizara ya mwaka wa fedha 2024/25.


xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Yasinta Kissima na William Mabusi – WKS Dodoma

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepokea na kuidhinisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Katiba na Taasisi zake kwa mwaka wa fedha 2024/25.

Akiwasilisha Bajeti hiyo, Waziri wa Katiba na  Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana  Bungeni Jijini Dodoma Aprili 29, 2024 amesema kuwa, katika mwaka wa fedha 2024/25  Wizara inataraji    kutumia jumla ya Shilingi Bilioni 441.26.

Akiwasilisha makadirio ya fedha kwa ajili ya kutekeleza mpango na Bajeti kwa mwaka wa fedha 2024/2025  Mhe. Balozi  Pindi Chana amesema kuwa kati ya fedha hizo Shilingi Bilioni 112.4  ni kwa ajili ya mishahara ya Watumishi, Shilingi Bilioni 223.16 ni kwa ajili ya matumizi mengineyo na Shilingi Bilioni 105.67 ni kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo.

Katika hotuba yake Dkt. Pindi Chana amesema kuwa kwa  mwaka wa fedha 2024/25 Wizara na Taasisi zake zitaendelea kuboresha utoaji wa huduma za Sheria na utoaji wa haki kwa umma ili kuendana na Mipango ya Sekta ya Sheria nchini na Mipango ya Kikanda na Kimataifa ili kufikia malengo yanayotarajiwa.



 

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA