WANANCHI LUPILA WAITWISHA MSLAC KERO YA WANYAMA WAHARIBIFU
Wakili wa Serikali kutoka Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Zakaria Mzese akitoa elimu ya Sheria kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Lupila katika Kata ya Lupila Mei 30, 2024 Makete. Afisa Wanyamapori kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Bw. Francis Malembo akitoa mada ya wanyamapori na makatazo kwenye Hifadhi za Taifa na Mapori Tengefu kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Lupila katika Kata ya Lupila Mei 30, 2024 Makete. Mwanasheria kutoka Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Fredrick Makamba akitoa mada ya ndoa na talaka kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Lupila katika Kata ya Lupila Mei 30, 2024 Makete. xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx William Mabusi – WKS Makete Wananchi wa Kijiji cha Lupila katika Kata ya Lupila Wilayani Makete wameitwisha Timu inayotekeleza Kampeni ya Kitaifa ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Wilayani humo kero ya wanyama nyani na ngedere ambao wamekuwa tishio kwa kuharibu mazao na kutishia amani. Malalamiko hayo yametolew...