ADHMA YETU NI KUENDELEA KUBORESHA UTOAJI HAKI – DKT. PINDI CHANA

 

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akiongea wakati anafungua Mkutano wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu, Mei 11, 2024 Jijini Dodoma.


Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akihutubia wakati anafungua Mkutano wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu, Mei 11, 2024 Jijini Dodoma.

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akisalimiana na baadhi ya Wabunge walioshiriki Mkutano wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu, Mei 11, 2024 Jijini Dodoma.


Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akiteta jambo na Wakili Onesmo Olengurumwa Mratibu wa Kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu kabla ya kuanza Mkutano wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu, Mei 11, 2024 Jijini Dodoma.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Na William Mabusi – WKS Dodoma

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amesema nia ya Serikali iliyoko madarakani inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuona Wananchi wanapata haki tena wanaipata kwa wakati. Katika kutimiza adhma hiyo Serikali imeendelea kuboresha utoaji haki, kuwa na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora na kuwa na Tume ya Haki Jinai.

Dkt. Chana ameyasema hayo wakati akifungua Mkutano ulioandaliwa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu kwa lengo la kujadili kwa pamoja masuala yanayogusa haki za binadamu, Mei 11, 2024 Jijini Dodoma.

Aidha, amesema Serikali itaendelea kutekeleza mikataba ya Kikanda na Kimataifa ya haki za binadamu, kuendelea kutoa elimu ya haki binadamu, wakati wote kuwa na sera za kutetea haki za binadamu na kuchukua hatua dhidi ya ukatili wa haki za binadamu.

Akiongelea ushirikiano na Watetezi wa hakli za Binadamu, Dkt. Chana amesema Serikali itaendelea kufanya kazi kwa pamoja na Mtandao wa Watetezi wa haki za binadamu kwa lengo moja la kuona Tanzania inaendelea kuwa na amani.


Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

UONGOZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU YAKUTANA NA VIONGOZI WA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

BODI YA KITAIFA YA USHAURI YA MSAADA WA KISHERIA YATEMBELEA WASAIDIZI WA KISHERIA IRINGA