KIPAUMBELE NI WILAYA AMBAZO HAZINA MAHAKAMA – SAGINI

 

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini akijibu maswali Bungeni, Mei 24, 2024, Dodoma.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Na William Mabusi – WKS Dodoma

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini amesema kipaumbele cha Serikali ni kujenga Mahakama kwenye Wilaya zote ambazo hazina Mahakama.

Mhe. Sagini ameyasema hayo leo Mei 24, 2024 Bungeni Dodoma alipokuwa anajibu swali la Mhe. Jonas Wiliam Mbunda Mbunge wa Mbinga Mjini aliyetaka kujua lini Serikali itajenga jengo la kisasa la Mahakama ya Wilaya ya Mbinga.

”Kulingana na ukubwa wa changamoto tulizonazo za uhaba na uchakavu wa majengo, kwa sasa, kipaumbele ni kujenga majengo ya Mahakama katika Wilaya ambazo hazina kabisa majengo ya Mahakama.” Alisema.

Mhe. Sagini amekiri kwamba jengo Mahakama ya Wilaya ya Mbinga  siyo la kisasa. Hata hivyo, jengo hilo bado lina hali nzuri kwa kuwa limekuwa likifanyiwa ukarabati mdogo mara kwa mara. Aidha, huduma za kimahakama zinatolewa bila changamoto katika jengo hilo ambalo limeunganishwa na Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano ili kuwezesha utoaji wa huduma kupitia mifumo ya kielektroniki inayotumiwa na Mahakama ikiwemo uendeshaji wa mashauri. 

Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

UONGOZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU YAKUTANA NA VIONGOZI WA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

BODI YA KITAIFA YA USHAURI YA MSAADA WA KISHERIA YATEMBELEA WASAIDIZI WA KISHERIA IRINGA