MSLAC YALIFIKIA GEREZA LA NJOMBE

 

Naibu Waziri Wizara ya Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini akipokea taarifa ya Gereza la Njombe. Katika ziara hiyo aliambatana na Katibu Mkuu wa Wizara Bi. Mary Makondo, Mkurugenzi wa Taifa wa Mashtaka Sylvester Mwakitalu, Wataalamu na Wadau wa Sheria ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (MSLAC) Mkoani Njombe. Mei 27, 2024.

Naibu Waziri Wizara ya Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini kwenye picha ya pamoja na  Katibu Mkuu wa Wizara Bi. Mary Makondo, Mkurugenzi wa Taifa wa Mashtaka Sylvester Mwakitalu, Wataalamu na Wadau wa Sheria mara baada ya kufika Gereza la Njombe kuzungumza na Wafungwa na Mahabusu  ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (MSLAC) Mkoani Njombe. Mei 27, 2024.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Na Hyasinta Kissima – WKS Njombe

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini amesema kuwa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia katika maeneo ya vizuizi ikiwemo Magereza imelenga kutimiza dhamira ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuona haki inatendeka kwa Watanzania wote na kwa wakati.

Mhe. Sagini ameyasema hayo Mei 27, 2024 wakati alipotembelea Gereza ya Njombe akiwa ameambatana na Katibu Mkuu wa Wizara Bi. Mary Makondo, Mkurugenzi wa Taifa wa Mashtaka Sylvester Mwakitalu, Wataalamu na Wadau wa Sheria  ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Mkoani Njombe.

"Yapo maeneo mbalimbali ambayo Kampeni hii imelenga kuyafikia ikiwemo Magereza ili kukabiliana na mapungufu  yanayoweza kuwa yamejitokeza katika usimamizi wa Sheria.Wafungwa na Mahabusu tulionao wanategemea washauriwe ipasavyo. Katika maeneo walipokwama na wengine mpaka wanahukumiwa msamaha wa Mhe. Rais unatoka lakini jamii haiwataki kuwapokea.Tunatengeneza mazingira gani ya usuluhishi lakini hata katika mazingira ya kudhaminiwa hata katika dhamana zilizo wazi Wananchi hawapo tayari kuwadhamini tunafanya nini ili wawe raia wazuri."Alisema Naibu Waziri Sagini.

Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo amesema kuwa Wizara kupitia mradi wa e-justice itawezesha upatikanaji wa vifaa kwa ajili ya mifumo ya kimtandao katika Mahakama, Magereza Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, Tume ya kurekebisha Sheria na wadau wengine kadri fedha zitakapokuwa zinapatikana.

Ikumbukwe kuw, tangu kuzinduliwa kwa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia mkoani Njombe Mei 26, 2024  timu za Wataalamu wa Sheria zinaendelea kutoa elimu na kutatua changamoto za Kisheria walizokuwa wanakabiliana nazo Wananchi katika Halmashauri  zote sita za mkoa wa Njombe na kuendelea  kuwafikia katika maeneo ya Magereza ili kuhakikisha haki inatendeka kwa kila Mtanzania.


Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

UONGOZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU YAKUTANA NA VIONGOZI WA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

BODI YA KITAIFA YA USHAURI YA MSAADA WA KISHERIA YATEMBELEA WASAIDIZI WA KISHERIA IRINGA