TUMEJIPANGA - MTAKA & CHANA

 

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akiongea na Wahabari kuhusu kufanyika kwa Kampeni ya Mama Samia mkoaji Njombe. Mei 22, 2024 Njombe. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka.

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka kwenye kikao na Wahabari kuhusu kufanyika kwa Kampeni ya Mama Samia mkoaji Njombe. Mei 22, 2024 Njombe.

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka kwenye picha ya pamoja na Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa baada kua kufanya kikao na Wanahabari kuhusu kufanyika kwa Kampeni ya Mama Samia mkoaji Njombe. Mei 22, 2024 Njombe.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Na Lusajo Mwakabuku – WKS Njombe

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka kwa pamoja wamesema wamejiandaa kikamilifu katika kuhakikisha kuwa wananchi wa Tanzania wananufaika na Kampeni ya Msaada wa Kisheria maarufu kama "Mama Samia Legal Aid Campaign"

Viongozi hao wameyasema hayo Mei 22, 2024 walipokuwa wakizungumza na Waandishi wa habari katika  ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe juu ya uzinduzi wa kampeni hiyo mkoani humo.

Utekelezaji wa Kampeni hiyo ulianzia jijini  Dodoma ambapo ilizinduliwa tarehe 27 Aprili, 2023, na Zanzibar tarehe 9 Mei, 2023.

Kwa sasa Kampeni hii imeufikia Mkoa wa Njombe ambapo huduma za msaada wa kisheria zitatolewa bure kwa Wananchi katika Halmashauri zote sita kuanzia tarehe 26 Mei, 2024.


Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

UONGOZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU YAKUTANA NA VIONGOZI WA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

BODI YA KITAIFA YA USHAURI YA MSAADA WA KISHERIA YATEMBELEA WASAIDIZI WA KISHERIA IRINGA