"TUWASAIDIE WANANCHI KUTATUA MIGORORO KUPITIA KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA YA MAMA SAMIA" – SAGINI

 

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini akizungumza  na washiriki wa mafunzo ya utoaji wa msaada wa kisheria (hawapo pichani) katika Kampeni ya Mama Samia Legal Aid Campaign, wakati aliposhiriki kwenye uzinduzi wa mafunzo ya siku moja yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji Njombe Mei 25, 2024.

Baadhi ya Wataalamu walioshiriki mafunzo ya utoaji wa Msaada wa Kisheria katika Kampeni ya Mama Samia Legal Aid Campaign, katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji Njombe Mei 25, 2024.

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini kwenye picha ya  pamoja na Wataalamu watakaoshiriki katika huduma za utoaji wa  msaada wa Kisheria katika Kampeni ya Mama Samia inayotarajiwa kuzinduliwa katika Mkoa wa Njombe Mei 26, 2024. Kushoto kwa kwake ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Khatibu Kazungu.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Hyasinta Kissima - WKS Njombe

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini amewataka Wataalamu watakaoshiriki katika zoezi la utoaji msaada wa kisheria katika Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia "Mama Samia Legal Aid Campaign" kuhakikisha wanatoa elimu kikamilifu ili kutatua migogoro na kero za Wananchi.

Mhe. Sagini ameyasema hayo Mei 25, 2024 katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji Njombe wakati akifungua mafunzo ya siku moja kwa Wataalamu watakaoshiriki katika zoezi la kutoa  msaada wa Kisheria kwa muda wa siku kumi katika Halmashauri sita za Mkoa wa Njombe.

"Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameanzisha Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia ili kuhakikisha kuwa kila Mwananchi ambaye hana uwezo wa kuwafikia Mawakili na Wanasheria kunufaika na huduma hii. Kampeni hii imekua na manufaa makubwa sana kwa Wananchi. Ninaamini ninyi mlioaminiwa kufanya kazi hii mtathamini uzito huu ambao Mhe. Rais ameuweka kupitia kampeni hii." Alisema Mhe. Sagini.

Katika hatua nyingine, Naibu Waziri Sagini ameelekeza ni vyema Wizara ya Katiba na Sheria ikaona umuhimu wa kufanya tafiti mbalimbali ili kuona madhara yatokanayo na watu kushindwa kufahamu haki zao Kisheria ambapo wakati mwingine malalamiko hayo huenda yakasababishwa na  Watumishi wa Umma wasiotimiza wajibu wao ipasavyo.

Tangu kuzinduliwa kwa Kampeni hiyo Kitaifa, Njombe ni Mkoa wa saba utakaoenda kunufaika na msaada huo wa Kisheria, na jumla ya Wataalamu 86 wamepatiwa mafunzo hayo watakaotoa msaada huo katika Halmashauri sita za Mkoa wa Njombe.



Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

UONGOZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU YAKUTANA NA VIONGOZI WA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

BODI YA KITAIFA YA USHAURI YA MSAADA WA KISHERIA YATEMBELEA WASAIDIZI WA KISHERIA IRINGA