DC NJOMBE AWATAKA WANANCHI KURIPOTI MIGOGORO KWA MSLAC

 

Mkuu wa Wilaya ya Njombe Mhe. Kissa Kasongwa akipokea nakala ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania  na vipeperushi kutoka kwa Wakili wa Serikali Mkuu Candid Nasua mara baada ya kutembelea banda la Wizara ya Katiba na Sheria Mei 31, 2024.

Huduma ya msaada wa Kisheria ikiendelea kutolewa katika banda la Wizara ya Katiba na Sheria ambapo Bi. Edith Shekidele, Wakili wa Serikali akitoa huduma ya Msaada wa Kisheria kwa mwananchi aitwae Leonard Hongoli.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Hyasinta Kissima – WKS Njombe

Mkuu wa Wilaya ya Njombe Mhe. Kissa Kasongwa amewataka Wananchi wa Wilaya ya Njombe kuhakikisha wanatumia uwepo wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia kutatua migogoro ya kisheria ambayo walikuwa wakiifikisha kwa viongozi hao  na  haikuweza kufikia muafaka.

Mheshimiwa Kissa ameyasema hayo Mei 31, 2024 wakati alipotembelea banda la Wizara ya Katiba na Sheria kwa lengo la kukagua shughuli zinazoendelea na kuzungumza na Wananchi waliokuwa wakipatiwa huduma mbalimbali za Kisheria katika banda hilo.

"Tunamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwani kupitia kampeni hii tumeanza kuona matokeo yake. Mfano tulikuwa na mgogoro wa Wananchi wa Lupembe Saccos lakini mpaka ninavyozungumza Madalali wapo kazini kukusanya madeni kwa waliokopeshwa kupitia Saccos na fedha hazijarudishwa."Alisema Kissa.

Aliendelea kusema "Niwaombe Wananchi wa Njombe kuhakikisha mnatumia kampeni ya Msaada wa Kisheria kutatua migogoro ya Kisheria ambayo mlikuwa mnaiwasilisha Ofisini. Wapo Mawakili na  Wataalamu wa Sheria hapa na huduma hizi ni bure. Watawashauri na kama mtahitaji Mawakili mtapatiwa bure."

Kwa upande wao baadhi ya Wananchi waliopatiwa huduma za Kisheria katika banda la Wizara na Wataalamu wa sekta hiyo akiwemo Leonard Hongoli wamesema kuwa ipo migogoro ambayo ilikuwa ikiwakabili lakini mara baada ya kuwasilisha maelezo ya migogoro hiyo kwa Wataalamu wa Sheria  wameweza kuelekezwa ni hatua gani za kufuata ili kuweza kuleta suluhu. 


Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA