DKT. GWAJIMA AONGOZA MKUTANO WA JUKWAA LA HAKI JINAI KAMATI YA MAWAZIRI
Waziri wa Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima akiongoza
Mkutano wa Jukwaa la Haki Jinai Kamati ya Mawaziri kama Mwenyekiti wa kikao
hicho kilichofanyika Juni 27, 2024 Kumbi za Bunge Jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Katiba na
Sheria Mhe. Jumanne Sagini akichangia mada kwenye Mkutano wa Jukwaa la Haki
Jinai Kamati ya Mawaziri uliofanyika Juni 27, 2024 Kumbi za Bunge Jijini
Dodoma.
Sehemu ya washiriki kwenye Mkutano
wa Jukwaa la Haki Jinai Kamati ya Mawaziri uliofanyika Juni 27, 2024 Kumbi za
Bunge Jijini Dodoma.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
William
Mabusi – WKS Dodoma
Waziri wa Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima ameongoza
Mkutano wa Jukwaa la Haki Jinai Kamati ya Mawaziri kwa leo kama Mwenyekiti wa
kikao hicho kilichofanyika Juni 27, 2024 Kumbi za Bunge Jijini Dodoma.
Katika Mkutano huo
uliotanguliwa na Kikao cha Makatibu Wakuu, pamoja na mambo mengine
wamejadili utekelezaji wa mapendekezo ya Tume ya Kuangalia jinsi ya kuboresha
Taasisi za Haki Jinai Nchini, Taarifa ya Jukwaa la Haki Jinai Taifa na Taarifa
ya ziara ya Mhe. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana alipotembelea
baadhi ya Magereza Nchini.
Comments
Post a Comment