PINDI CHANA AFUNGUA MAFUNZO YA MAKATIBU TAWALA WA WILAYA

 

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akihutubia kwenye Kikao Kazi cha Mafunzo kwa Makatibu Tawala wa Wilaya kuhusu shughuli za Usajili wa Matukio Muhimu ya Kibinadamu, Juni 27, 2024 Njombe.

Afisa Mtendaji Mkuu na Kabidhi Wasii Mkuu wa RITA Bw. Frank K. Frank akitoa taarifa ya utangulizi kwenye Kikao Kazi cha Mafunzo kwa Makatibu Tawala wa Wilaya kuhusu shughuli za Usajili wa Matukio Muhimu ya Kibinadamu, Juni 27, 2024 Njombe.

Baadhi ya Washiriki kwenye Kikao Kazi cha Mafunzo kwa Makatibu Tawala wa Wilaya kuhusu shughuli za Usajili wa Matukio Muhimu ya Kibinadamu, Juni 27, 2024 Njombe.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Na Mwandishi Wetu - Njombe

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana leo Juni 27, 2024 amefungua mafunzo kwa Makatibu Tawala wa Wilaya kuhusu shughuli za Usajili wa Vizazi, Vifo, Ndoa, Talaka na Udhamini yaliofanyika katika ukumbi wa Agreement  mkoani Njombe.

Mhe. Pindi Chana akifungua mafunzo hayo amesisitiza juu ya umuhimu wa Usajili wa matukio muhimu ya binadamu kama vizazi, vifo na sababu zake, ndoa na talaka kwani takwimu hizo zinasaidia Serikali katika kupanga maendeleo.

“Tumekuwa tukizitumia takwimu hizi katika kupanga mipango mbalimbali ya  maendeleo na huduma kwa jamii, hivyo natoa maelekezo kwa Ofisi zote za Mikoa ndani ya Tanzania Bara ziwe zinaandaa taarifa za robo mwaka za usajili wa matukio muhimu ya Binadamu ambazo zitabainisha Mafanikio na changamoto na kuziwasilisha RITA ili ziweze kufanyiwa kazi.” Alisema.



Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA