SERIKALI KUENDELEA KUSIMAMIA HAKI ZA WATOTO – DKT. CHANA
Sehemu ya Washiriki kwenye Mdahalo
kuhusu Sera za ajira kwa Watoto, Juni 05, 2024 Jijini Dar es Salaam.
xxxxxxxxxxxxxxxxx
Waziri wa Katiba na Sheria
Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana leo Juni 05, 2024 jijini Dar es Salaam amefungua
mdahalo kuhusu Sera za ajira kwa watoto uliolenga kuimarisha ulinzi wa watoto katika kuelekea kukomesha
utumikishwaji wa Watoto Tanzania.
Akizungumza katika mdahalo huo
Mhe. Chana amesema kuwa Serikali itaendelea kusimamia haki za watoto na hatua
kali zitachukuliwa kwa wote wanaokiuka sheria inayomlinda mtoto.
Chana ameongeza kuwa kila
mmoja ana wajibu wa kumlinda mtoto kwa nafasi yake.
"Wajibu wetu kila mmoja
kwa nafasi yake kuhakikisha mtoto analindwa, Wazazi nyumbani, Viongozi wa Dini,
Walimu mashuleni na jamii kwa ujumla tushirikiane na Serikali tuhakikishe mtoto
analindwa." Alisema.
Mdahalo huo unalenga kujadili
uboreshaji wa Sera na Sheria mbalimbali zinazomlinda mtoto kukomesha
utumikishwaji wa watoto kwenye ajira na kuelimisha jamii juu
ya haki za Watoto.
Comments
Post a Comment