SHERIA ZA UANGALIZI WA UTAJIRI ASILI NA MALIASILIA ZA NCHI KUHUISHWA
Waziri wa Katiba na Sheria
Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akiongea baada ya kupokea taarifa ya maandalizi ya
rasimu ya Mkakati wa mwaka 2024 – 2029 wa utekelezaji wa Sheria za Uangalizi wa
utajiri asili na Maliasilia za nchi Sura 449 na 450. Juni 24, 2024 Ofisi za
Bunge Dodoma.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Uangalizi
wa Utajiri Asili na Maliasilia za Nchi DCP Neema Mwanga (mwenye laptop), akitoa
taarifa ya maandalizi ya rasimu ya Mkakati wa mwaka 2024 – 2029 wa utekelezaji
wa Sheria za Uangalizi wa utajiri asili na Maliasilia za nchi Sura 449 na 450, tarehe
24 Juni, 2024 ofisi za Bunge Dodoma.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Na
William Mabusi – WKS Dodoma
Waziri wa Katiba na Sheria
Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amepokea taarifa ya maandalizi ya rasimu ya Mkakati
wa mwaka 2024 – 2029 wa utekelezaji wa Sheria za Uangalizi wa utajiri asili na
Maliasilia za nchi Sura 449 na 450.
Mkakati huo wenye lengo la kuhakikisha
kuwa uvunaji na matumizi ya utajiri asili na Maliasilia za nchi unazingatia
maslahi ya Taifa na Maendeleo endelevu ya wananchi, umewasilishwa na Mkurugenzi
wa Kitengo cha Uangalizi wa Utajiri Asili na Maliasilia za Nchi DCP Neema Mwanga,
tarehe 24 Juni, 2024 ofisi za Bunge Dodoma.
Mkakati wa awali wa
utekelezaji wa sheria tajwa wa mwaka 2019 umemaliza muda wake mwaka 2021/22. Mkakati
wa sasa ni Jumuishi na utatekelezwa na Wizara, Idara na Taasisi zinazojihusisha
na masuala ya utajiri asili na Maliasilia za nchi. Aidha, Mkakati huo
utazingatia misingi ya Sheria tajwa pamoja na Sera na Sheria zingine ambazo ni
msingi wa umiliki na udhibiti wa utajiri asili na maliasilia.
Comments
Post a Comment