SERIKALI YAELEZA JISI TANZANIA ILIVYOJIPANGA KUPAMBANA NA MATUKIO YA UKATILI KWA WATU WENYE UALBINO.

 

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana pamoja na ujumbe wa Tanzania walipofanya mazungumzo kwa njia ya mtandao na Mtaalam wa kujitegemea anayehusika na masuala ya Haki za watu wenye ualbino Bi. Muluka-Anne Miti-Drummond, Julai 4, 2024 Geneva.

xxxxxxxxxxxxxx

Na Lusajo Mwakabuku – WKS Geneva

Tanzania imekuwa ni nchi inayotazamwa zaidi na mashirikia mbalimbali ya kimataifa yanayohusika na Haki za Binadamu hususan Matukio ya ukatili kwa watu wenye ualbino ambayo yameendelea kujitokeza mara kwa mara.

Hayo yameelezwa na Bi. Muluka-Anne Miti-Drummond ambaye ni mtaalam wa kujitegemea anayehusika na masuala ya Haki za watu wenye ualbino alipofanya mazungumzo kwa njia ya mtandao (Zoom Meeting) na Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Hazara Chana leo tarehe 04/07/2024.

Akielezea suala hilo, Bi Muluka-Anne amesema linapofika suala la ukatili wa watu wenye ualbino nchi ya Tanzania imekuwa ikishika nafasi ya juu kuandikwa katika vyombo mbalimbali vya Habari na hata mitandao ya kijamii, suala lililowafanya wao kuiangalia Tanzania kwa jicho la kipekee yanapokuja masuala yanayohusu watu wenye ualbino nchini.

Bi. Muluka akasema suala hilo limezua taharuki miongoni mwa wazazi ambao watato wao wana ualbino kiasi wanashindwa hata kuwaacha waende shule wakihofia usalama wao na suala hili kwao limekuwa changamoto kubwa wakati wakiandika ripoti kwani wanashindwa kushauri jinsi ya kuwalinda watu wenye ualbino kwani kuwaweka katika sehemu maalumu ni kuwanyima haki ya kuishi na familia zao.

Akijibu hoja hizo, Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Hazara Chana alisema Tanzania inafanya juhudi kubwa katika kuhamasiha jamii jinsi ya kuondokana na imani potofu ambayo ndio inasemekana kuwa chanzo kikubwa cha ukatili huu kwa kupitia njia mbalimbali zikiwemo vyombo vya Habari, mikutano ya hadhara na vyombo vya dini kama Makanisa na Misikiti katika maeneo mbalimbali.

Aidha, Pindi Chana alieleza kuwa Tanzania inasimamia ipasavyo sheria hususan zile zinazohusika na masuala ya ubaguzi na kwamba hili suala limetengenezewa mkakati wa kitaifa na hivi karibuni Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa Majaliwa akizungumza Bungeni amesema hatua ya kuwalinda watu wenye ualbino ni jambo linalopaswa kutelelezwa na makundi yote ya jamii na kwa upande wake Serikali imeweka hatua kadhaa ambazo utekelezaji wake utahusisha wakuu wa mikoa, wilaya, vyombo vya dola, viongozi wa dini pamoja na watoa tiba za jadi.

Pamoja na jitihada hizo, Pindi chana alieleza kuwa Serikali inahakikisha upatikanaji wa vikingajua ikiwa ni pamoja na kutoa kodi kwenye uingizaji wa dawa na vifaa ambavyo watu wenye ualbino wanavipata.


Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA