TANZANIA IMEWEKA MIKAKATI YA KUPAMBANA NA UMASKINI – PINDI CHANA

 

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akichangia mjadala kwenye Kikao cha 56 cha Baraza la Haki za Binadamu kinachoendelea katika Ofisi za Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa Geneva, Switzerland. Julai 2, 2024.

XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

Na Lusajo Mwakabuku – WKS Geneva

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amesema Serikali ya Tanzania imeweka mikakati mbalimbali katika kuhakikisha inaondoa wimbi la umaskini uliokithiri katika jamii ambao hupelekea maskini kupata Haki za kibinadamu kwa kiasi kidogo au kutozipata kabisa.

Waziri  Chana amesema hayo leo tarehe 02/07/2024 alipokuwa akichangia mjadala unaohusu umaskini uliokithiri na jitihada za kuutatua katika kikao cha 56 cha Baraza la Haki za Binadamu kinachoendelea katika Ofisi za Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa Geneva, Switzerland.

Waziri Chana amesema Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inafuata msingi wa maendeleo unaozingatia haki za binadamu,  maisha bora, utulivu wa amani na umoja, utawala bora, kuwa na jamii iliyoelimika na yenye uchumi imara wenye ushindani ni baadhi ya sifa kuu za Dira  ya Maendeleo ya 2025.

“Pia tuko katika mchakato wa kuendeleza DIRA yetu ya maendeleo ya 2050 ambayo ni mchakato shirikishi unaowaleta pamoja Watendaji wa Serikali na Wasiokuwa wa Serikali ili kuhakikisha hakuna anayeachwa nyuma katika ajenda ya maendeleo”. Aliongeza Pindi Chana

Waziri Chana alihitimisha mchango wake kwa kuelezea  jinsi Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilivyofanya Sensa ya Kitaifa ya Watu na Makazi mwaka 2022 ikiwa ni nyenzo ya kimkakati itakayotumika wakati wa kuandaa mpango wa maendeleo wa DIRA 2050 unaolenga kukomesha umaskini na kukuza haki za binadamu kwa kuzingatia Maendeleo Endelevu.


Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA