TATHMINI YA UKARABATI JENGO LA USULUHISHI IKAMILIKE KWA WAKATI

 

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini (kulia) akiteta jambo na baadhi ya Wakurugenzi kutoka Wizara ya Katiba na Sheria walipotembelea jengo linalotarajiwa kutumika kama Kituo cha Usuluhishi lililopo Temeke,  jijini Dar es Salaam. Julai 6, 2024.

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini (kulia) pamoja na baadhi ya Viongozi kutoka Wizara ya Katiba na Sheria wakitembelea jengo linalotarajiwa kutumika kama Kituo cha Usuluhishi lililopo Temeke,  jijini Dar es Salaam. Julai 6, 2024.

xxxxxxxxxxxxx

Hyasinta Kissima – WKS Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini Julai 6, 2024 akiwa ameambatana na baadhi ya Wakurugenzi  kutoka Wizara ya Katiba na Sheria wametembelea katika jengo linalotarajiwa kutumika kuwa Kituo cha Usuluhishi kilichopo Temeke,  jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri Sagini ameelekeza kuharakishwa kwa kazi ya kufanyika kwa  tathmini ya ukarabati wa jengo hilo inayofanywa na TBA ili ukarabati ukamilike kwa wakati na jengo hilo lianze kutumika.

Aidha, Mhe. Sagini ameelekeza Sekretarieti ya Kituo cha Usuluhishi kianze kuandaliwa mapema ili jengo litakapokuwa limekamilika lianze kufanya kazi mara moja.


Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA