UKAGUZI UNAONGEZA THAMANI KATIKA KUTOA HUDUMA BORA KWA WANANCHI - MAKONDO


 Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo akizungumza katika kikao cha ufunguzi wa kazi ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali za Wizara ya Katiba na Sheria kwa mwaka 2023/2024, katika ukumbi wa Wizara Mtumba jijini Dodoma, Julai 15, 2024.


Msaidizi wa Mkaguzi  Mkuu wa Serikali Esnath Nicodem (wa kwanza kulia) akiwasilisha taarifa ya Kaguzi zitakazofanyika ambapo Kaguzi za hesabu za Serikali  za  Wizara ya Katiba na Sheria kwa mwaka 2023/2024.


Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo akiongoza kikao kilichowahusisha Wakaguzi wa Nje kutoka Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali na Timu ya Menejimenti ya Wizara  kilichofanyika katika ukumbi wa Wizara Mtumba, jijini Dodoma, Julai 15, 2024.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Hyasinta Kissima- WyKS

Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo amesema kuwa  kaguzi mbalimbali zinazofanywa na Serikali katika Taasisi zake  zimewezesha kuboresha utoaji huduma na kuongeza thamani na ubora wa huduma mbalimbali zinazotolewa na Taasisi hizo  kwa Wananchi wake.

Bi. Makondo ameyasema hayo Julai 15, 2024 wakati wa kikao cha ufunguzi wa kazi ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali  za  Wizara ya Katiba na Sheria kwa mwaka 2023/2024, kilichowahusisha Wakaguzi wa Nje kutoka Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali na Timu ya Menejimenti ya Wizara  kilichofanyika katika ukumbi wa Wizara Mtumba, jijini Dodoma.

"Tunashukuru kwa kuweza kutupitisha  katika taarifa ya Kaguzi ambazo mnataraji kuzifanya kwa kipindi mtakapokuwepo hapa kwani kupitia Kaguzi mnazozifanya tunapata mwongozo wa namna bora ya kuwahudumia Wananchi. Wizara itawapatia ushirikiano wa kutosha katika kukamilisha Kaguzi zenu ikienda sambamba na upatikanaji wa nyaraka katika utekelezaji wa majukumu mahsusi.” Alisema Katibu Mkuu.

Awali, Msaidizi wa Mkaguzi  Mkuu wa Serikali Esnath Nicodem akiwasilisha taarifa ya Kaguzi zitakazofanyika amesema kuwa, Kaguzi ya kwanza itahusisha Taasisi ya RITA ambapo ukaguzi utakaofanyika utalenga kuangalia ufanisi wa utendaji  katika maeneo ya Usajili Ufilisi na Udhamini kwa kipindi cha miaka mitatu ikiwa ni mwaka (2021/2022, 2022/2023, /2023/2024 pamoja na ukaguzi wa hesabu za Serikali  za  Wizara ya Katiba na Sheria kwa mwaka 2023/2024. 

Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA