WAZIRI CHANA AFANYA MAZUNGUMZO NA NAIBU KAMISHNA MKUU WA HAKI ZA BINADAMU WA UMOJA WA MATAIFA

 

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana alipofanya mazungumzo na Naibu Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu Bi. Nada Yousseff Al Nashif, Julai 3, 2024 Geneva.

Naibu Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu Bi. Nada Yousseff Al Nashif, kwenye mazungumzo na Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana, Julai 3, 2024 Geneva.

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana na ujumbe wa Tanzania kwenye picha ya pamoja na Naibu Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu Bi. Nada Yousseff Al Nashif, Julai 3, 2024 Geneva.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Na Lusajo Mwakabuku – WKS Geneva

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Hazara Chana akiambatana na ujumbe kutoka Tanzania amefika katika ofisi za Naibu Kamishna Mkuu za Umoja wa Mataifa zilizopo Geneva na kufanya mazungumzo na Bi. Nada Yousseff Al Nashif - Naibu Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu juu ya utekelezwaji wa Haki za Binadamu nchini Tanzania.

Katika mazungumzo hayo, yaliyofanyika Julai 3, 2024 Waziri Chana alielezea kwa kina juu ya suala malalamiko ambayo Naibu Kamishna Mkuu alisema bado wanaendelea kuyapokea na kuyajadili kuhusu kuhamishwa kwa nguvu kwa watu asilia (wamasai) katika maeneo ya Ngorongoro na kusema kuwa kuwa Serikali iliamua kufanya maamuzi hayo kwa kuwa Wananchi wa Ngorongoro walikuwa hawawezi kumiliki ardhi, kujenga makazi bora na ya kudumu na kufanya mambo  yao ya maendeleo kwa ajili ya mustakabali wa familia zao kwa kuwa yalikuwa yanakinzana na Sheria ya Uhifadhi.

Mbali na hilo, Dkt. Pindi Chana amemweleza Kamishna huyo  kuwa wananchi wanaoishi Ngorongoro  wamekuwa wakikumbana na kadhia nyingi ambapo kuna wananchi ambao wameuawa na wanyamapori wakali na waharibifu na wengine walijeruhiwa na wanyamapori hao na kuwasababishia vilema vya kudumu.

Ameelezea kuwa wananchi waliohamia kijiji cha Msomera wamelipwa fidia, wamejengewa nyumba zenye staha pamoja na kupewa hati ya kumiliki ardhi pamoja na kupatiwa huduma zote za kijamii ambazo walipokuwa Ngorongoro walizikosa

”Serikali imeendelea kuwapa stahiki zao  wananchi wote wanaohama kwa hiari ikiwa ni pamoja na kuwapa fidia inayostahili pamoja na kuwasafirishia mizigo,  mali na mifugo yao kuelekea kwenye makazi mapya na huu ndo msingi wa haki za binadamu” amesisitiza Mhe. Balozi Dkt. Pindi chana.

Ameongeza kuwa “Wananchi wa Ngorongoro hususan watoto kwa kipindi kirefu  walikosa haki ya kupata elimu bora, haki ya kuishi bila woga na haki ya kucheza kutokana na hofu ya kushambuliwa na wanyamapori wakali na waharibifu hivyo kitendo cha kuhamia Msomera watoto hao watapata haki zao  za msingi kama ilivyo kwa watoto wa maeneo mengine.”



Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA