WIZARA YAITA WADAU UBORESHAJI WA DAFTARI LA ORODHA YA WATOA HUDUMA ZA MSAADA WA KISHERIA

 

Msajili wa Watoa Huduma za Msaada wa Kisheria Bi. Ester Msambazi akiwasilisha rasimu ya daftari la orodha ya watoa huduma wa Msaada wa kisheria kwa wadau walioshiriki uboreshaji wa Daftari la Orodha ya Watoa Huduma za Msaada wa Kisheria. Julai 16, 2024 Dodoma.


Mdau Maiko Salali kutoka asasi ya Foundation for Disability Hope akichangia katika mjadala wa kuboresha Daftari la Orodha ya Watoa Huduma za Msaada wa Kisheria leo tarehe 16/07/2024.

Leonard Haule ambaye anatokea TAKUKURU lakini pia ni mwakilishi wa Chama cha Mawakili wa Serikali akichangia katika mjadala wa kuboresha Daftari la Orodha ya Watoa Huduma za Msaada wa Kisheria leo tarehe 16/07/2024.


Baadhi ya wadau wa kikao cha kuboresha Daftari la Orodha ya Watoa Huduma za Msaada wa Kisheria wakifuatilia wasilisho la rasimu ya daftari la orodha ya watoa huduma wa Msaada wa kisheria leo tarehe 16/07/2024 Mtumba Jijini Dodoma.

xxxxxxxxxxxxxxxxx

Lusajo Mwakabuku – WyKS Dodoma.

Wizara ya Katiba na Sheria leo tarehe 16/07/2024 imeitisha kikao cha wadau kujadili uboreshaji wa Daftari la Orodha ya Watoa Huduma za Msaada wa Kisheria linalotarajiwa kuzinduliwa rasmi mwishoni mwa mwezi wa nane, 2024.

Kikao hicho kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Katiba na Sheria Mtumba Dodoma, kimejumuisha wataalam kutoka taasisi za Serikali na Asasi za Kiraia kimeazimia kuunda timu maalum ambayo itatengeneza daftari lenye taarifa bora zaidi na kuliwasilisha katika Menejiment ya Wizara kabla ya kuzinduliwa rasmi.

Lengo la daftari hili ni kusogeza zaidi huduma kwa wananchi ili pale mwananchi atakapohitaji huduma za Msaada wa Kisheria kutosafiri  umbali mrefu kufuata huduma hizo Wizarani na  badala yake kutumia daftari hilo kufahamu ni sehemu gani katika eneo alilopo kuna huduma na aina ya msaada anayoweza kupata. 


Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA