DKT. CHANA AWASILISHA MUSWADA WA MAREKEBISHO YA SHERIA YA SHULE YA SHERIA KAMATI YA BUNGE
Waziri wa Katiba na Sheria
Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akiwasilisha Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya
Shule ya Sheria mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na
Sheria, katika ukumbi mdogo wa Bunge jijini Dodoma, Agosti 14, 2024.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba
na Sheria Bw. Eliakim Maswi akichangia hoja wakati wa kujadili Muswada wa
Marekebisho ya Sheria ya Shule ya Sheria mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Utawala, Katiba na Sheria, katika ukumbi mdogo wa Bunge jijini Dodoma, Agosti
14, 2024.
Kikao cha Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa wasilisho la Muswada wa
Marekebisho ya Sheria ya Shule ya Sheria, katika ukumbi mdogo wa Bunge jijini
Dodoma, Agosti 14, 2024.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Waziri wa Katiba na Sheria
Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akiwasilisha Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya
Shule ya Sheria Sura ya 425 (THE LAW SCHOOL ACT CAP 425) mbele ya Kamati ya
Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, katika ukumbi mdogo wa Bunge jijini
Dodoma, Agosti 14, 2024.
Muswada huo unapendekeza
kufanya Marekebisho katika Sheria husika kwa lengo la kukabiliana na changamoto
mbalimbali zilizobainika katika utekelezaji wa masharti ya Sheria.
Comments
Post a Comment