MASWI AFANYA MAZUNGUMZO NA MSHAURI ELEKEZI WA BSAAT
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Eliakim Maswi (wa
tatu kulia) kwenye picha ya pamoja na wajumbe walioshiriki kikoa na Mshauri
Elekezi wa Programu ya BSAAT, Agosti 13, 2024 Ofisi za Wizara Mtumba Dodoma.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba
na Sheria Bw. Eliakim Maswi, 13 Agosti 2024, amekutana na kufanya
mazungumzo na Mshauri Elekezi wa Programu ya Kujenga Uwezo wa Taasisi katika
kupambana na rushwa (Building Sustainable Anti- Corruption Action in Tanzania -
BSAAT).
Katika mazungumzo hayo
yaliyofanyika katika Ofisi za Wizara Mtumba jijini Dodoma, taarifa
ya utekelezaji wa programu hiyo iliwasilishwa na kujadili maeneo ya
mashirikiano kati yao na Wizara katika kutekeleza mapendekezo ya
Tume ya Haki Jinai.
Comments
Post a Comment