PINDI CHANA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA USAJILI WA WATOTO DODOMA

 




xxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Na Lusajo Mwakabuku - WyKS Dodoma

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana leo Agosti 09, 2024 amefanya ziara na kukagua zoezi la usajili na kuwapatia vyeti vya kuzaliwa watoto wa umri chini ya miaka mitano katika hospitali ya St. Gemma, Kituo cha afya Makole na Zahanati ya  Kikuyu Jijini Dodoma.

Katika ziara hiyo Waziri Chana, amewataka wananchi kuhakikisha watoto wao wanasajiliwa na kupatiwa vyeti vya kuzaliwa mara baada ya kujifungua kabla ya kuruhusiwa kurudi nyumbani.

"Ndugu Wananchi hasa kina mama wenzangu, Serikali yetu inayoongozwa na Mhe. Rais Mama Samia Suluhu Hassan imewaletea huduma hii ya vyeti vya kuzaliwa bure kwa watoto wetu hivyo hii ni fursa kwenu kwani vyeti hivyo vitawasaidia kupata huduma ya matibabu kupitia bima ya afya, baadaye elimu na ajira." Alisema.

Pia Waziri Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana aliwakabidhi vyeti vya kuzaliwa baadhi ya akina mama waliojifungua salama na kuruhusiwa katika vituo hivyo vya tiba.

Akizungumza kwa niaba ya Wanawake waliokuwa   wakipatiwa huduma hiyo Bi. Halima Abdallah ameishukuru Serikali kwa kuwasogezea huduma hiyo na kuahidi kuwa balozi kwa kuwaelimisha ndugu, marafiki na majirani kuhusu upatikanaji wa huduma hiyo na umuhimu wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto.


Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA