Prof. KABUDI AWASILISHA MUSWADA WA MAREKEBISHO YA SHERIA YA SHULE YA SHERIA
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa
Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akimpongeza Waziri wa Katiba na Sheria Mhe.
Palamagamba Kabudi (Mb) kwa kuaminiwa na kuteuliwa kuwa Waziri wa Katiba na
Sheria na pia kwa kuwasilisha Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Shule ya Sheria Sura ya 425 (THE LAW
SCHOOL ACT CAP 425) katika kikao cha kwanza cha Mkutano wa 16
wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Agosti 27,
Bungeni jijini Dodoma.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bw. Hamza Johari akila Kiapo cha Uaminifu Bungeni na kukabidhiwa vitendea kazi na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson Agosti 27, 2024 kabla ya kuanza kwa kikao cha kwanza cha Mkutano wa 16 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bungeni, jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya
Katiba na Sheria, Bw. Eliakim Maswi (kulia) akizungumza na Naibu
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bw. Samwel Maneno (kushoto) pamoja na baadhi
ya Wakuu wa Taasisi zilizopo chini ya Wizara hiyo muda mfupi kabla ya kuapishwa
kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bw. Hamza Johari Agosti 27, 2024
Bungeni jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Bw. Eliakim
Maswi (wa kwanza kushoto) akiwa pamoja na baadhi ya Wakuu wa Taasisi zilizopo
chini ya Wizara na baadhi ya Wakurugenzi wa Idara mbalimbali za Taasisi hizo
wakifuatilia kikao cha kwanza cha Mkutano wa 16 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Agosti 27, Bungeni jijini Dodoma.
Comments
Post a Comment