SERIKALI INARIDHISHWA NA KAZI ZA WASULUHISHI

 

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Abdallah Sagini akisoma hotuba kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi katika Mkutano wa Mwaka wa Taasisi ya Wasuluhishi Tanzania (Tiarb) uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hotel ya Protea Malliot jijini Dar es salaam, tarehe 23/08/2024.

Rais wa Taasisi ya Usuluhishi Tanzania (TIArb), Madeline Kimei akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Abdallah Sagini aliyemwakilisha Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi katika Mkutano wa Mwaka wa Saba wa  Taasisi ya Wasuluhishi Tanzania (Tiarb), 23/08/2024.

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Abdallah Sagini akiwa meza kuu katika Mkutano wa Mwaka wa Taasisi ya Wasuluhishi Tanzania (Tiarb) uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hotel ya Protea Malliot jijini Dar es salaam tarehe 23/08/2024.

           Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Abdallah Sagini akifuatilia matukio katika Mkutano wa Mwaka wa Taasisi ya Wasuluhishi Tanzania (Tiarb) uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hotel ya Protea Malliot jijini Dar es salaam, tarehe 23/08/2024.


Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Abdallah Sagini na viongozi wa Tiarb na baadhi ya wanachama wakiwa katika picha ya pamoja, tarehe 23/08/2024

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Na Lusajo Mwakabuku  -  WyKS Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Abdallah Sagini amesema Serikali inaridhishwa na juhudi zinazofanya na taasisi mbalimbali zinazoshughulikia masuala ya upatanishi kwenye migogoro mbalimbali hususan migogoro ya biashara.

Mhe. Sagini ameyasema hayo tarehe 23/08/2024 alipokuwa akimwakilisha Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi katika Mkutano wa Mwaka wa Taasisi ya Wasuluhishi Tanzania (Tiarb) uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hotel ya Protea Malliot jijini Dar es salaam.

Akiwasilisha salamu za Waziri Kabudi, Mhe. Sagini alisema migogoro inayomalizika nje ya Mahakama inatumia muda mfupi kuliko ile inayofuata taratibu za  kimahakama ambayo mara nyingi upande mmoja hasa ule ulioshindwa  unabaki na maumivu yanayopelekea kujengeka kwa uhasama baina ya pande hizo mbili.

“Tukiweza kuweka juhudi za pamoja katika kuimarisha matumizi ya njia mbadala za utatuzi wa migogoro tutaweza kufanikisha malengo ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (1977) ya kutochelewesha haki bila sababu ya kimsingi [Ibara ya 107A (2) (b)]; kukuza na kuendeleza usuluhishi baina ya wanaohusika katika migogoro [Ibara ya 107A (2) (d)]; na kutenda haki bila kufungwa kupita kiasi na masharti ya kiufundi yanayoweza kukwamisha haki kutendeka [Ibara ya 107A (2) (e)]” alisema Mhe. Sagini.

Akizitaja faida hizo, Mhe. Sagini alisema matumizi ya njia hizi mbadala huharakisha upatikanaji wa haki kwa haraka na kwa watu wote, huokoa muda na gharama za wadaawa ambazo zinaweza kutumika katika uzalishaji wa uchumi. Pia njia hizi mbadala zina faida nyingine kubwa kama vile ushiriki wa wenye mgogoro katika kutafufa suluhu wao wenyewe, kuwepo kwa usiri na faragha kwa wadaawa, kutumia njia zisizo na utaratibu mgumu ambazo hukubalika kwa pande zote mbili pamoja na kuhifadhi mahusiano baina ya wadaawa.

Aidha Mhe. Sagini aliongeza kuwa Matumizi ya Usuluhishi yanafaida kubwa ya kupandisha hadhi na nafasi ya Tanzania katika ripoti ya hali ya uwekezaji urahisi wa kufanya biashara inayoweka viwango vya kimataifa katika upimaji wa mfumo wa ushughulikiaji wa migogoro ya madai.

“Sote tutambue usuluhishi ni dhana yenye kututaka tubadili fikra zetu za utoaji haki zilizojengwa na mfumo wa utoaji haki unaochukua muda mrefu kabla ya mgogoro kumalizika kwa kufuata ngazi za kimahakama kuanzia Mahakama za Mwanzo hadi ya Rufani, na kupitia katika hatua nyingi, maahirisho mengi na mapingamizi mengi ya kiufundi ndani ya kila ngazi za Mahakama”. Alihitimisha Mhe. Sagini.


Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA