Posts

Showing posts from September, 2024

KATIBA NA SHERIA NA UONGOZI WA TLS WAKUBALIANA KUSHIRIKIANA

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akiongea katika kikao na Baraza la Uongozi la Chama cha Mawakili wa Tanzania (TLS) Mtumba Dodoma katika Ofisi za Wizara ya Katiba na Sheria 17/09/2024. Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Eliakim Maswi akiongoza majadiliano ya wataalam baina na Menejimenti ya Wizara na Uongozi wa TLS kabla ya kumkaribisha Waziri wa Katiba na Sheria. 17/09/2024. Rais wa TLS Bw. Boniface Mwabukusi akielezea kufurahishwa kwake na mapokezi tangu walipowasili Wizara ya Katiba kabla ya kuanza kuelezea hoja za ushirikiano. 17/09/2024. Baadhi ya viongozi kutoka Baraza la Uongozi la Chama cha Mawakili wa Tanzania (TLS) wakifuatilia majadiliano katika kikao hicho. 17/09/2024. Menejimenti ya Wizara na Uongozi wa TLS waliohudhuria katika kikao hicho wakifuatilia majadiliano. 17/09/2024. Waziri wa Katiba na Sheria, Menejimenti ya Wizara na Uongozi wa TLS wakiwa katika picha ya pamoja. 17/09/2024. xxxxxxxxxxxxxxxxx Na Lusajo Mwakabuku & Hyasi

KABUDI AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA MKUTANO WA AALCO THAILAND.

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba J. A. Kabudi aongoza ujumbe kutoka Tanzania nchini Thailand kushiriki Mkutano Mkuu wa 62 wa Shirika la Mashauriano ya Kisheria wa Kimataifa wa Nchi za Asia na Afrika (AALCO). Septemba 11, 2024 Thailand. xxxxxxxxxxxxxxxxxxx Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba J. A. Kabudi, Septemba 11, 2024 amekutana na kufanya mazungumzo na Mhe. Polcol Tawee Sodsong, Waziri wa Sheria wa Thailand ambapo pamoja na mambo mengine wamezungumzia maeneo ya ushirikiano hususan kuwa na programu za mafunzo na kubadilishana uzoefu katika masuala ya sheria za uwekezaji na sekta ya sheria kwa ujumla. Waziri Kabudi anaongoza ujumbe kutoka Tanzania nchini Thailand unaoshiriki Mkutano Mkuu wa 62 wa Shirika la Mashauriano ya Kisheria wa Kimataifa wa Nchi za Asia na Afrika (AALCO).

MOCLA YAZINDUA KITUO CHA HUDUMA KWA MTEJA

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi akihutubia katika hafla ya uzinduzi wa Kituo cha Huduma kwa Mteja, Septemba 05, 2024 Mtumba Jijini Dodoma. Mkurugenzi wa Idara Katiba na Ufuatiliaji Haki Bi. Jane Lyimo akitoa neno la utangulizi kwa niaba ya Katibu Mkuu Bw. Eliakim Maswi katika hafla ya uzinduzi wa Kituo cha Huduma kwa Mteja, Septemba 05, 2024 Mtumba Jijini Dodoma. Mkurugenzi Kitengo cha Uangalizi wa Utajiri wa Asili na Maliasili za Nchi DCP Neema Mwanga akitoa neno la ukaribisho kwa Wageni waliofika kwenye hafla ya uzinduzi wa Kituo cha Huduma kwa Mteja, Septemba, 2024 Mtumba Jijini Dodoma. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Kituo cha Huduma kwa Mteja, Septemba, 2024 Mtumba Jijini Dodoma. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi akimsikiliza na kumhudumia mwananchi kutokea Wilaya ya Uyui Mkoani Tabora aliyepiga simu katika Kituo cha Huduma kwa Mteja akiuliza kuhusu usimamizi wa mirathi,