PROF. KABUDI AFANYA KIKAO NA BALOZI WA URUSI NCHINI

 



xxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi leo 27 Septemba, 2024 jijini Dar es Salaam amekutana na kufanya kikao na Balozi wa Urusi Nchini Bw. Andrey Avetisyan kujadili maeneo mbalimbali ya kiuchumi na kidiplomasia kwa lengo la kuleta maendeleo kwa jamii.

Akizungumza katika kikao hicho Mhe. Kabudi amesema kuwa mbali na urafiki na ushirikiano uliopo baina ya Nchi hizi mbili wanaendelea kuangalia maeneo muhimu ya kuboresha ikiwemo ushirikiano kwenye masuala mbalimbali ikiwemo la utoaji wa huduma za haki ambalo liko chini ya mamlaka ya Wizara ya Mambo ya Katiba na Sheria, elimu, utamaduni, ulinzi, utalii, afya, biashara na uwekezaji.

Aidha Bw. Avetisyan amesema kuwa Urusi itaendelea kushirikiana na Tanzania ili kuimarisha zaidi mahusiano yaliyopo ili kuboresha upatikanaji wa haki na kupambana na uhalifu kwa njia ya mtandao.


Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

UONGOZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU YAKUTANA NA VIONGOZI WA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

BODI YA KITAIFA YA USHAURI YA MSAADA WA KISHERIA YATEMBELEA WASAIDIZI WA KISHERIA IRINGA