Posts

Showing posts from October, 2024

KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA KUFANYIKA MIKOA MINNE KWA PAMOJA

Image
  Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Msaada wa Kisheria Bi. Ester Msambazi akifungua mafunzo kwa Viongozi wa Makundi (Team Leaders) katika ukumbi wa Hotel ya Edema Morogoro mjini tarehe 17/10/2024. Wakili wa Serikali kutoka Katiba na Sheria Bw. Candid Nasua akifanya wasilisho katika mafunzo kwa Viongozi wa Makundi (Team Leaders) yatakayotoa msaada wa kisheria katika kampeni ya MSLAC katika ukumbi wa Hotel ya Edema Morogoro mjini tarehe 17/10/2024. Baadhi ya washiriki wa mafunzo kwa Viongozi wa Makundi (Team Leaders) yatakayotoa msaada wa kisheria katika kampeni ya MSLAC wakifuatilia wasilisho katika ukumbi wa Hotel ya Edema Morogoro mjini tarehe 17/10/2024. xxxxxxxxxxxxxxxxxxxx Wizara ya Katiba na Sheria ipo katika hatua za mwisho za maandalizi ya kuendeleza utekelezaji wa kampeni ya msaada wa kisheria katika Mikoa Minne ambayo ni Mororgoro, Iringa, Songwe na Mara. Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Msaada wa Kisheria Bi. Ester Msambazi wakati akimwakilisha Katib

WAZIRI KABUDI APOKEA TAARIFA NANE ZA MAPITIO YA SHERIA

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi akiongea wakati wa hafla ya kukabidhiwa taarifa nane za tafiti za mapitio ya Sheria zilizofanywa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2023/2024 kutoka Tume ya Kurekebisha Sheria Nchini (LRCT), 16 Oktoba, 2024. Mtumba jijini Dodoma. Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Nchini (LRCT) Mhe. Jaji Winfrida Korosso akiongea wakati wa hafla ya kukabidhi taarifa nane za tafiti za mapitio ya Sheria zilizofanywa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2023/2024 na Tume hiyo, 16 Oktoba, 2024. Mtumba jijini Dodoma. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi akipokea taarifa nane za tafiti za mapitio ya Sheria  zilizofanywa kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2023/2024 na Tume ya Kurekebisha Sheria Nchini (LRCT) kutoka kwa Mwenyekiti  wa Tume hiyo Mhe. Jaji Winfrida  Korosso, 16 Oktoba, 2024. Mtumba jijini Dodoma. xxxxxxxxxxxxxxxxxxxx Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi amepokea taarifa nane za tafiti za mapitio

WIZARA YATOA MOTISHA

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi akikabidhi kiasi cha shilingi milioni sita kwa Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mhe. Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu ikiwa ni utekelezaji wa ahadi iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Wizara Bw. Eliakim Maswi wakati alipotembelea makao makuu ya Tume ikiwa ni sehemu ya motisha kwa ajili ya Watumishi wawili waliofanya kazi katika Tume kwa zaidi ya miaka thelathini. 15 Oktoba, 2024 Ofisi za Wizara Mtumba jijini Dodoma.

WAZIRI KABUDI AHIMIZA USHIRIKIANO KWA TAASISI ZINAZOSIMAMIA HAKI JINAI

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akizungumza na Menejimenti ya Taasisi zinazounda Utatu wakati akifungua kikao cha Utatu Oktoba 9, 2024 jijini Dodoma. Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bw. Sylvester Mwakitalu akizungumza katika kikao cha Utatu, 10 Oktoba, 2024 Jijini Dodoma. Baadhi ya Wakuu wa  Taasisi zinazounda Utatu pamoja na Wakuu wa Mashtaka Mikoa, Wakuu wa Upelelezi Mikoa na Wakuu wa TAKUKURU Mikoa wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi wakati akifungua kikao cha Umoja huo tarehe 9 na 10 Oktoba, 2024 Jijini Dodoma. xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi amezitaka taasisi zinazosimamia masuala ya Haki Jinai kuhakikisha kuwa wanasimamia  na kuendeleza umoja na mshikamano waliouanzisha unaojulikana kama Utatu, ili kuongeza weledi na ufanisi katika kulinda Haki za watu wote kwa kufuata misingi ya Katiba na Sheria. Waziri Kabudi amebainisha hayo tarehe 9 Oktoba, 2024 j

KABUDI MGENI RASMI MHADHARA WA KUMBUKUMBU YA BENJAMINI MKAPA

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akitoa salamu za ufunguzi katika Mhadhara maalum wa Hayati Benjamini Mkapa, Rais wa Awamu ya Tatu ulioandaliwa na Chuo Kikuu Cavendish cha Uganda, Oktoba 01, 2024 katika ukumbi wa hotel ya Johari Rotana Jijini Dar es salaam. xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx Na Lusajo Mwakabuku - WyKS Dar Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi ameshiriki kama Mgeni Rasmi katika Mhadhara maalum wa Hayati Benjamini Mkapa, Rais wa Awamu ya Tatu ulioandaliwa na Chuo Kikuu Cavendish cha Uganda leo tarehe 01/10/2024 katika ukumbi wa hotel ya Johari Rotana Jijini Dar es salaam. Akitoa salamu za ufunguzi katika mhadhara huo, Waziri Kabudi alisema kwake hii ni fursa adhimu kuhutubia mkutano huu unaosherehekea maisha ya kiongozi aliyekuwa na maadili na mchapakazi na kwamba kumbukumbu ya Benjamin Mkapa ina nafasi ya pekee katika mioyo ya wengi kwani inatuwezesha kutafakari juu ya uongozi na maono ya mtu ambaye maono yake yalivuka mipak