KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA KUFANYIKA MIKOA MINNE KWA PAMOJA


 Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Msaada wa Kisheria Bi. Ester Msambazi akifungua mafunzo kwa Viongozi wa Makundi (Team Leaders) katika ukumbi wa Hotel ya Edema Morogoro mjini tarehe 17/10/2024.


Wakili wa Serikali kutoka Katiba na Sheria Bw. Candid Nasua akifanya wasilisho katika mafunzo kwa Viongozi wa Makundi (Team Leaders) yatakayotoa msaada wa kisheria katika kampeni ya MSLAC katika ukumbi wa Hotel ya Edema Morogoro mjini tarehe 17/10/2024.

Baadhi ya washiriki wa mafunzo kwa Viongozi wa Makundi (Team Leaders) yatakayotoa msaada wa kisheria katika kampeni ya MSLAC wakifuatilia wasilisho katika ukumbi wa Hotel ya Edema Morogoro mjini tarehe 17/10/2024.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Wizara ya Katiba na Sheria ipo katika hatua za mwisho za maandalizi ya kuendeleza utekelezaji wa kampeni ya msaada wa kisheria katika Mikoa Minne ambayo ni Mororgoro, Iringa, Songwe na Mara.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Msaada wa Kisheria Bi. Ester Msambazi wakati akimwakilisha Katibu Mkuu wa Katiba na Sheria katika kufungua mafunzo ya siku tatu kwa wataalam kutoka taasisi mbalimbali za kisheria ambao ndio watakuwa viongozi wa timu zitakazotoa huduma ya Msaada wa Kisheria katika mikoa tajwa.

 

Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA