"MAJAJI NA WAENDESHA MASHTAKA WAJENGEWE UWEZO KUENDESHA MASHAURI DHIDI YA BIASHARA HARAMU YA BINADAMU" - MASWI

 

Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Eliakim Maswi (katikati) akizungumza katika kikao kilichowakutanisha wataalam kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na ujumbe kutoka Nchini Marekani wanaohusika na mapambano na ufuatiliaji dhidi ya biashara ya usafirishaji haramu wa Binadamu. Tarehe 30 Oktoba, 2024 ofisi za Wizara Mtumba, Dodoma.

Ofisa kutoka Ofisi inayoshughulika utokomezaji na ufuatiliaji wa biashara ya usafirishaji haramu wa Binadamu kutoka nchini Marekani Bw. Adam Blakeman amesema kuwa  Nchi ya Tanzania ni miongoni mwa Nchi zilizopiga  hatua kubwa katika mapambano dhidi ya biashara hiyo ukilinganisha na Nchi nyingine barani Afrika.


xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Eliakim Maswi amesema Nchi ya Tanzania imefanya jitihada mahususi katika kupambana na usafirishaji haramu wa Binadamu ikiwemo marekebisho ya Sheria mbalimbali na adhabu kali kwa watuhumiwa wa biashara hiyo, licha ya  uhaba wa rasilimali fedha na uwezo mdogo wa Wataalam wa kada  mbalimbali wakiwemo  Majaji na Waendesha Mashtaka wenye Elimu ya Mapambano dhidi ya biashara hiyo.

Bw. Maswi amesema hayo katika kikao cha kubadilishana uzoefu wa mbinu zinazoweza kutumika dhidi ya Usafirishaji haramu wa Binadamu kilichowakutanisha wataalam kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Ujumbe kutoka Nchini Marekani wanaohusika na mapambano dhidi ya usafirishaji haramu wa Binadamu kilichofanyika tarehe 30 Oktoba, 2024 katika ukumbi wa Wizara Mtumba jijini, Dodoma.

Maswi ameeleza kuwa ili kuweza kuendana na wakati na kudhibiti biashara hiyo, Majaji na Waendesha Mashtaka ni miongoni mwa kada zinazotakiwa kujengewa uwezo ambapo takwimu zinaonesha kuwa Waendesha Mashtaka wanne waliopo  kwenye kikosi kazi cha mapambano hayo ndiyo waliojengewa uwezo kuhusiana na Mapambano hayo.

"Biashara ya Usafirishaji Haramu wa Binadamu ni biashara inayowahusisha watu wenye fedha, hivyo hata mapambano yake yanahitaji uwezo wa kifedha. Kwa upande wa Wizara ya Katiba na Sheria yapo maeneo ambayo Wataalam wake wanahitaji kujengewa uwezo wakiwemo Majaji na Waendesha Mashtaka ili kuweza kuwa na uelewa mpana na kuendesha mashauri  yanayohusiana na biashara hiyo." Alisema Katibu Mkuu.

Kwa upande wake Ofisa kutoka Ofisi inayoshughulika Utokomezaji  na ufuatiliaji wa biashara ya usafirishaji haramu wa Binadamu kutoka Nchini Marekani Bw. Adam Blakeman amesema kuwa  Nchi ya Tanzania ni miongoni mwa Nchi zilizopiga  hatua kubwa katika mapambano dhidi ya biashara hiyo ukilinganisha na Nchi nyingine barani Afrika.



Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

UONGOZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU YAKUTANA NA VIONGOZI WA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

BODI YA KITAIFA YA USHAURI YA MSAADA WA KISHERIA YATEMBELEA WASAIDIZI WA KISHERIA IRINGA