TUME YA TEC YAKUTANA NA KABUDI NA KATAMBI

 

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi  akifafanua jambo katika kikao hicho pembeni yaka ni Mhe. Patrobas Katambi, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu walipokutana na Tume ya TEC Mtumba Dodoma leo 07/11/2024.

Baadhi ya wawakilishi wa Tume ya Kimisionari ya Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki (TEC) wakiongozwa na Mwenyekiti wa Tume hiyo Askofu Damian Dallu (Wa kwanza Kuala) wakifuatilia mazungumzo hayo.

Mhe. Patrobas Katambi, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu akichangia hoja katika mazungumzo hayo.

Jopo la wawakilishi wa Tume ya Kimisionari ya Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki (TEC) kwenye picha ya pamoja na Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi na Mhe. Patrobas Katambi, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu pamoja na wajumbe wa menejimenti ya Wizara ya Katiba na Sheria.

Mwenyekiti wa Tume ya Kimisionari ya Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki (TEC) Askofu Damian Dallu akifafanua jambo katika kikao hicho.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Jopo la wawakilishi wa Tume ya Kimisionari ya Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki (TEC) limekutana na Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi na Mhe. Patrobas Katambi, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu kuzungumzia juu ya taarifa ya takwa la marekebisho ya sheria kuhusu wamisionari wa kikatoliki Tanzania wenye uraia wa nje.

Mazungumzo hayo yanafuatia ombi lililotolewa na Askofu Mkuu wa Songea na Mwenyekiti wa Tume ya Kimisionari ya Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki (TEC) Askofu Damian Dallu kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alipofanya ziara ya kikazi na kufanya mazungumzo na viongozi wa dini mjini Songea mwishoni mwa mwezi Septemba mwaka huu Mkoani Ruvuma.

Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Katiba na Sheria Mtumba leo tarehe 07/11/2024 na kushuhudiwa na Katibu Mkuu Bwana Eliakim Maswi na baadhi ya wajumbe wa Menejimenti ya Wizara.





Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

UONGOZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU YAKUTANA NA VIONGOZI WA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

BODI YA KITAIFA YA USHAURI YA MSAADA WA KISHERIA YATEMBELEA WASAIDIZI WA KISHERIA IRINGA